Watangaza Nia CCM Waendelea Kusaka Wadhamini; Lowassa, Wasira na Membe…!

Mh. Lowassa, akipokea fomu zilizojazwa na wana CCM waliomdhamini mkoani Shinyanga, kutoka kwa katibu wa CCM wilaya ya Shin yanga mjini Charles Sangula, Juni 11, 2015.

Mh. Lowassa, akipokea fomu zilizojazwa na wana CCM waliomdhamini mkoani Shinyanga, kutoka kwa katibu wa CCM wilaya ya Shin yanga mjini Charles Sangula, Juni 11, 2015.

Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, akisalimiana na motto mwenye ulemavu wa ngozi, Kabula Zacharia, anayetunzwa kwenye kituo cha kulea watu wenye ulemavu wa ngozi cha Buhangija mkoani Shinyanga, mara baada ya kupata wana CCM
wa kumdhamini kufuatia kuchukua fomu za kuomba chama kimteue kuwania urais wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.  Lowassa amabaye yuko kanda ya ziwa kutafuta wadhamini, alivunja rekodi ya kupatya wadhamini 7,114, idadi kubwa hadi sasa. (Picha na K-VIS MEDIA)

 

Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, akipungia mkono wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Shinyanga,
alipokuwa akiondoka ofisi za chama hicho wilaya ya Shinyanga mjini mara baada ya kupata wana CCM wa kumdhamini baada ya kuchukua fomu kuomba CCM imteue kugombea urais kwenye uchaguzi mkuu wa Tanzania unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Lowassa amabaye yuko kanda ya ziwa kutafuta wadhamini, alivunja rekodi ya kupatya wadhamini 7,114, idadi kubwa hadi sasa. 

 

Furaha ya kumuona Mh. Lowassa, ilitawala ukumbi mzima

 

 

 

Wananchi wa mkoa wa Shinyanga, wakisukumana ili wapiti
kumuona Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, alkipokuwa akiwasili kwenye ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga mjini Juni 11, 2015, ili kuomba wanachama wenzake wa chama hicho wamdhamini kufuatia kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa na chama hicho, kuwania urais wa Tanzania Oktoba 25, 2015

 

Wana CCM walkiofika kumdhamini Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, wakishangilia wakati akiingia ukumbi wa CCM wilaya ya Shinyanga mjini Juni 11, 2015. Lowassa amabaye yuko kanda ya ziwa kutafuta wadhamini, alivunja rekodi ya kupatya wadhamini 7,114, idadi kubwa hadi sasa

 

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (kulia) akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Njombe, waliofika kwenye Ofisi ya CCM Wilaya ya Njombe Jana, kwa ajili ya kutia saini fomu za kumdhamini ili ateuliwe kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, ambapo aliweza kupata wadhamini zaidi ya 360.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Iringa, waliofurika kwenye Ofisi ya CCM Wilaya ya Iringa mjini Jana, kwa ajili ya kutia saini fomu za kumdhamini ili ateuliwe kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, ambapo aliweza kupata wadhamini 317.
 Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wasira akiongea na baadhi ya wanachama wa CCM mkoani Mtwara alipofika kuomba kudhaminiwa
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wasira akipokewa na baadhi ya wanachama wa CCM mkoani Mtwara alipofika kuomba kudhaminiwa 
Na Woinde Shizza
WAZIRI wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wasira,amewahimiza wakazi wa Mtwara kuwekeza katika uzalishaji wa mazao ya kilimo na uvuvi ikiwa ni sehemu ya shughuli za kiuchumi zitakazowanufaisha kutokana na kugundulika kwa gesi asilia katika ukanda wa kusini mwa nchi.
Wasira ambaye pia ni Mbunge wa Bunda alikuwa akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  aliomdhamini ili apitishwe na chama hicho kuwania Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Alisema ingawa zipo fursa nyingi zitakazowanufaika
Watanzania  kutokana na sekta hiyo mpya
(gesi), lakini mazao ya kilimo na uvuvi yanaweza kuwa miongoni mwa shughuli
zitakazowanufaisha wananchi wengi hasa wa hali ya chini.
Mtwara ni eneo lililowahi kukumbwa na machafuko kutokana
na hisia tofauti zilizokuwapo kuhusu manufaa yanayopaswa kuwafikia wakazi wa
mkoani Mtwara, hasa kuhusu ujenzi wa viwanda na kuibadili gesi ili
itakaposafirishwa isiwe katika mali ghafi.
Hata hivyo, Wasira alisema anatarajia kufungua fursa
nyingi zaidi za kiuchumi kwa ajili ya wananchi kama atateuliwa na CCM na
hatimaye kushinda katika Uchaguzi huo.
Hakuelezea kwa undani kutokana na kuwa wakati wa kampeni
bado haujafika, bali sasa hivi anatafuta udhamini ndani ya CCM.
Wakati huo, Wasira na mtia mwingine, Makongoro Nyerere,
wameelezea kuridhika na namna wanavyoshiriki mchakato wa kusaka Urais kwa
kutumia magari, tofauti na watia nia waliowekeza fedha nyingi kiasi cha kutumia
usafiri wa angani katika maeneo mengi.
Waliyasema hayo walipokutana kwenye ofisi za CCM mkoa wa
Mtwara, ambapo Makongoro, alirukaruka na kumkumbatia Wasira. Tukio hilo lilitafsiriwa
kuwa ni ishara za umuhimu wa kufanya ushawishi kwa amani pasipo kuiathiri CCM,
wanachama ama Watanzania kwa ujuma.
“Hizi ndizo siasa tunazozitaka ndani ya CCM na Tanzania
yetyu, sio wagombea wengine wanaotumia utajiri na fedha zao kuwakandamiza
wadogo na kuibua mafarakano kwenye jamii,” akasikika kiongozi mmoja wa CCM
(jina tunalo) akisema.
Wasira, alikwenda pia katika mkoa wa Lindi ambapo
alifadhiliwa. Leo (alhamis) ataelekea mkoani Mwanza kuendelea na ziara ya
kuomba udhamini kwa wana-CCM wa mikoa ya kanda ya Ziwa Victoria.