Vitabu Milioni 2.5 Vyasambazwa Kwa Shule za Sekondari Nchini

Rais Kikwete akikabidhiwa vitabuBalozi wa Marekani nchini, Mark Childress (kushoto), akimkabidhi Rais Jakaya Kikwete sehemu ya vitabu ikiwa ni ishara ya makabidhiano ya vitabu milioni 2.5 vya sayansi na hisabati vilivyotolewa na serikali ya Marekani kwa ajili ya shule za sekondari za serikali nchini katika hafla iliyofanyika Shule ya Sekondari Mtakuja Beach iliyopo Manispaa ya Kinondoni Dar es Salaam leo. Hafla hiyo ilifanyika katika shule hiyo kwa niaba ya shule zote za serikali nchini. Vitabu hivyo tayari vimesambazwa katika shule hizo nchini.

 

 Wananchi waliojitokeza katika sherehe ya makabidhiano ya vitabu milioni 2.5 vya sayansi na hisabati kwa shule za sekondari za serikali nchini. Vitabu hivyo kutoka  serikali ya watu wa Marekani vilikabidhiwa kwa Rais Jakaya Kikwete na Balozi wa Marekani nchini, Mark Childress katika hafla iliyofanyika Shule ya Sekondari Mtakuja Beach iliyopo Manispaa ya Kinondoni Dar es Salaam leo. Hafla hiyo ilifanyika katika shule hiyo kwa niaba ya shule zote za serikali nchini.
 Rais Jakaya Kikwete na Balozi wa Marekani nchini, Mark Childress wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mtakuja Beach huku wakiwa wameshika baadhi ya vitabu walivyokabidhiwa katika sherehe hiyo.
 Rais Jakaya Kikwete akimkabidhi vitabu hivyo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa.
 Balozi wa Marekani nchini, Mark Childress akihutubia 
kwenye hafla hiyo.
 Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mtakuja Beach wakishangilia katika sherehe hiyo.
 Wanawake wakicheza wimbo wa Christian Bela wa Mama.
 Wadau wa elimu wakiwa kwenye hafla hiyo.
 Wanawake wakishangilia wakati Rais Jakaya Kikwete 
akiwasili kwenye sherehe hizo.
 Mkuu mpya wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akiteta jambo na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk.Shukuru Kawambwa wakati wakimsubiri Rais Kikwete awasili.
 Meya wa Manispaa ya Kinondoni Yusuf Mwenda (kulia), akitoa taarifa ya shughuli za maendeleo katika sekta ya elimu mbele ya Rais Jakaya Kikwete.
Rais Kikwete akiwa na viongozi wengine baada ya kuwasili kwenye sherehe hizo. Kutoka ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Sadiki na Balozi wa Marekani nchi, Mark Childress.
Wasanii wa Kikundi cha Utamaduni cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), wakitoa burudani katika hafla hiyo. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)