Viongozi wa Chadema Lyamgungwe Wamfuata Mgimwa CCM

Mbunge wa Jimbo la Kalenga (CCM), Godfrey Mgimwa akikagua moja ya miradi ya maendeleo jimboni kwake.

Mbunge wa Jimbo la Kalenga (CCM), Godfrey Mgimwa akikagua moja ya miradi ya maendeleo jimboni kwake.

 

Mbunge  wa  jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa kulia akipokea kadi ya Chadema  kutoka kwa mmoja kati ya  viongozi wa Chadema   kata ya Lyamgungwe  aliyehamia CCM.

Wananchi  wa Lyamgungwe  wakiwa  wameongozana na mbunge wake  kwenda kutembelea  miradi ya maendeleo
Kada  wa Chadema  kulia akipongezwa na mbunge Mgimwa baada ya  kujiunga na CCM
Mbunge Mgimwa akizungumza na  wananchi  wake baada ya  kupokea  wana chama wa Chadema

Na MatukiodaimaBlog

VIONGOZI watatu wa vyama vinavyounda katiba ya  wananchi (UKAWA) Kata ya Lyamgungwe Jimbo la Kalenga wamempongeza mbunge wa  jimbo la hilo, Godfrey Mgimwa kwa kutekeleza ahadi mbalimbali zilizoachwa na marehemu mbunge aliyepita Dk. Wiliam Mgimwa kwa muda mfupi na kuwa katika kuonyesha umoja wao wameamua  kuunganisha  nguvu zao  kwa
mbunge huyo kwa kuhama Chadema na  kujiunga na CCM.
 
Akizungumza kwa niaba ya wanachama wenzao zaidi ya 20 ambao  walikuwa nyuma yao kabla ya kujiengua Chadema na kujinga na CCM   walisema kuwa sababu ya kujiunga na upinzani ilitokana na makundi  ndani ya CCM na upendeleo wa uteuzi wa wagombea mbalimbali pamoja na wabunge waliotangulia  kuonyesha kutumia ubunge kulea  familia  zao badala ya kuleta maendeleo  katika jimbo  hilo jambo ambalo mbunge Mgimwa amekuwa wa  tofauti  na  wabunge wengine kwa kuonyesha  kuwajali  zaidi  wapiga kura wake.
 
Bw. Mapinduzi Kalolo  ambae  alikuwa ni viongozi  wenzake  wengine
waliorudi CCM ni  pamoja na katibu kata, mwenyekiti na wajumbe na  kuwa kujiunga kwao  Chadema  ni baada ya mambo  ndani ya CCM kutokwenda vizuri  ila kwa  sasa  mbunge  wao  ameendelea  kuwaunganisha wananchi  wote  bila  kujali itikadi zao  za  vyama.
 
Pia alisema  walipotoka CCM kwenda  Chadema walikuwa wameahidiwa mambo mengi na viongozi wa Chadema jimbo  hilo la Kalenga ila baada  ya kujiunga utekelezaji wa ahadi  walizotoa ikiwemo ya  kufungua ofisi
ilionekana na ngumu na kuwa  chama  hicho hata  kuwajali kilishindwa na
hivyo kuishia  kuonekana si chochote katika kata  hiyo zaidi ya
kutumika kama karai na Chadema.
 
“Kujiunga na  Chadema  kweli  tulikuwa  tumepotea  ila  kwa  sasa  tumeona  ni vema  kurudi  kwa  baba na mama CCM baaba  ya maisha ya  kuishi kama mwana mpotevu  kutushinda…hivyo tunakuhakikishia  mheshimiwa mbunge Mgimwa wewe  ndio  umetushawishi  kuhama  Chadema na kujiunga na CCM kutokana na kuonyesha mfano katika kutekeleza ahadi  zao kwa wananchi…kalenga hatujapata  kuwa na mbunge ambae  amefanya mambo makubwa kama wewe  ndani ya  miezi minne …haya  uliyofanya  wewe wabunge wengine  walikuwa  wakishindwa  kuyafanya kwa  kipindi  cha miaka 5  ya  ubunge.”
 
Hata
hivyo  Kalolo  alisema  kuwa  ni matumaini makubwa  kwao  kuwa  kazi
iliyofanywa na mbunge Mgimwa kwa  kipindi  kifupi  cha miezi  minne
ama  cha mwaka  mmoja wa utawala  wake ni imani  tosha kwao kwa
kuendelea  kumchagua  zaidi kwa  miaka mingine 10  mbele  ili
kuliwezesha  jimbo  hilo  kuwa la mfano zaidi.
 
HIvyo
alikitaka   CCM kuacha tabia ya  viongozi  wake wa  wilaya  kuwaruhusu
baadhi ya  wana CCM kuzunguka  kuwavuruga wapiga  kura  kwa  kubeza
jitihada  zinazofanywa na mbunge  Mgimwa na kuwa kufanya  hivyo ni
kukaribisha upinzani katika   jimbo  hilo.
 
Kalolo
alisema  iwapo  viongozi wa CCM ngazi ya  wilaya na mkoa  watashikamana
na mbunge  Mgimwa upo  uwezekano  wa upinzani kufutwa kabisa katika
jimbo  hilo ambalo halijapata  kuwa na historia ya  kuongozwa na
upinzani.
 
 
Kwa upande  wake  aliyekuwa  mwenyekiti  wa  Jimbo  la  Kalenga kupitia
Chadema  Dk. Salum Kalolo  alisema  kuwa  kuondoka kwa viongozi hao
Chadema na  kujiunga  na CCM kutokana na utendaji wa  mbunge  huyo
Mgimwa hawajakosea kwani kwa  mtazamo  wake  kazi inayofanywa na mbunge huyo jimboni inapaswa  kuungwa mkono na  kila mwananchi bila kujali itikadi ya chama chake.
Wengi  walijua kuwa  kutokana na ujana  wake  mambo ya maendeleo
yasingeweza  kusonga mbele  ila mimi  si CCM mimi ni Chadema kutoka
sakafu ya  moyo  wangu  ninampongeza munge Mgimwa  amekuwa mbunge wa mfano katika  kutuletea maendeleo Kalenga,”
 
Zipo
changamoto  mbali mbali ambazo iwapo  atapewa  muda  wake wa kipindi
japo  kimoja cha miaka 5  kuanzia mwakani 2015  tungependa atusaidie
kutatua  ni pamoja na adha  ya maji na uboreshaji wa  shule za msingi
ambazo nyingi  hazipo katika hali nzuri.
 
Hata
hivyo mbunge  Mgimwa alisema malengo  yake ni  kuweka rekodi  nzuri ya
ubunge katika  jimbo  hilo la Kalenga na kulifanya kuwa  jimbo lenye
maendeleo makubwa  ikiwa ni pamoja  na kuona ndoto  yake ya kuanzisha
benki ya  wananchi wa Kalenga  inaanzishwa  ili  kusaidia  kuwakopesha
wakulima mitaji.
 
Kuhusu
suala la maji alisema  tayari katika baadhi ya maeneo ameanza
kutekeleza ahadi ya  maji  safi pamoja na kupeleka  umeme katika kata ya
Mgama na Magulilwa ili  kuchochea kasi ya maendeleo japo  maombi  yake
kwa  wananchi ni  kuendelea  kumwombea  zaidi  ili ndoto  yake ya kuleta
maendeleo ifanikiwe zaidi.