UWT Mufindi Wampigia Magoti Bi. Mkini Kugombea Ubunge

Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mufindi Bi Marcelina Mkini wa kwanza kushoto akiwa na mkuu wa wilaya ya Mufindi Mboni Mhita na mwenyekiti wa UWT mkoa wa Iringa Bi Zainabu Mwamwindi wakati wa kongamano la wanawake wilayani Mufindi.

Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mufindi Bi Marcelina Mkini wa kwanza kushoto akiwa na mkuu wa wilaya ya Mufindi Mboni Mhita na mwenyekiti wa UWT mkoa wa Iringa Bi Zainabu Mwamwindi wakati wa kongamano la wanawake wilayani Mufindi.

Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mufindi Bi Marcelina Mkini wa kwanza kushoto akiwa na mkuu wa wilaya ya Mufindi Mboni Mhita na mwenyekiti wa UWT mkoa wa Iringa Bi Zainabu Mwamwindi wakati wa kongamano la wanawake wilayani Mufindi.

Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mufindi Bi Marcelina Mkini wa kwanza kushoto akiwa na mkuu wa wilaya ya Mufindi Mboni Mhita na mwenyekiti wa UWT mkoa wa Iringa Bi Zainabu Mwamwindi wakati wa kongamano la wanawake wilayani Mufindi.

Mwenyekiti wa UWT Mufindi na mjumbe wa NEC Taifa, Bi Marcelina Mkini akiwapongeza  wanawake kwa kumkubali

 WAKATI joto  la Uchaguzi  Mkuu likiendelea  kushika kasi ndani ya Chama  Cha Mapinduzi (CCM) kwa  wanachama  wake kujitokeza kutia nia kuwania nafasi ya urais, ubunge na udiwani, umoja  wa wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Mufindi umemuomba Mwenyekiti wa umoja huo Wilaya ya Mufindi, Marcelina Mkini kugombea ubunge Jimbo la Mufindi  Kusini.

Wakizungumza mara baada ya  kumalizika kwa Kongamano la UWT Wilaya ya Mufindi wajumbe wa kongamano  hilo  walisema  kuwa  toka nchi ipate  uhuru  wake  mwaka 1961  wilaya ya Mufindi mkoani Iringa haijapata  kuwa na mbunge mwanamke  hivyo kwa uchaguzi wa mwaka  huu lazima wanawake wachukue nafasi ya  kuongoza ubunge jimbo la Mufindi kusini ambalo kwa  sasa  linaongozwa na mbunge Mendrady Kigola (CCM).

Akizungumza kwa  niaba ya  wenzake mjumbe wa UWT Mufindi Bi Anna Nyamba kutoka  kijiji  cha Nyololo  alisema  kuwa wamevutiwa na utendaji kazi  wa mwenyekiti  wao Bi Mkini na  kuwa wamepata  kuwa na wenyeviti  wengi  wa UWT ndani ya wilaya ya Mufindi ila hawakuweza  kuifanya  jumuiya hiyo  kuwa hai kama  ilivyo  sasa .

Hivyo  alisema kazi nzuri  iliyoonyeshwa na mwenyekiti  huyo ndani ya UWT kuna  uwezekano mkubwa zaidi wananchi  wa  jimbo la Mufindi kusini iwapo  watamchagua kuwa mbunge  wa  jimbo  kasi ya maendeleo  inaweza  kuongezeka  zaidi .

Bi Nyambo  alisema  kipimo cha  utendaji wa mwenyekiti huyo ni katika nafasi yake ya  ujumbe  wa NEC Taifa  akiwakilisha  wilaya ya Mufindi japo kazi mbali mbali za  kimaendeleo alizozifanya kwa  kukiwezesha chama cha mapinduzi kuwa hai kupitia jumuiya  hiyo ya UWT ni kielelezo  tosha kuwa  iwapo atakubali  kugombea  ubunge na  kushinda nafasi hiyo sura  mpya ya maendeleo itaonekana katika  wilaya ya Mufindi.

“…Sisi kama UWT Mufindi tutamuunga mkono mwanamke  mwenzetu ambae kazi zake  zimeonekana katika nafasi hii ya ubunge…leo jimbo letu halina barabara za uhakika na tunaopata shinda ni  wanawake na  watoto huduma za maji jimboni hakuna hivyo  tunataka kuwapa  wanawake watuongoze ,”

Bi  Aida Kaduma mjumbe  kutoka  kijiji  cha Lufuna kata ya Mtwango alisema kuwa uwezekano  wa Marcelina  kuwatumikia  wananchi wa jimbo la Mufindi  kusini ni mkubwa kwani tayari kuna kazi nyingi za kimaendeleo ambazo amepata  kushirikiana na  wananchi  kuzitekeleza kama mwenyekiti  wa UWT wilaya  hiyo .

Alisema kwa upande wa kijiji chake shule ya msingi Lufuna ilikuwa haina  nyumba ya mwalimu mkuu ila kwa  jitihada  zake aliweza kuchangia bati  zote 40 za kuezekea nyumba  hiyo na  sasa nyumba  hiyo  imekamilika na mwalimu anaishi .

Pia  alisema mbali ya kusaidia sekta ya  elimu amepata  kuchangia taasisi mbali mbali za kiserikali na dini katika jimbo la Mufindi ambako amepata  kualikwa kama mgeni rasmi na  kuwa matumaini ya wanawake Mufindi  kusini ni kuona wanawake wanachukua nafasi ya ubunge. Kwa  upande wake mwenyekiti  huyo Bi Mkini mbali ya  kuwapongeza wajumbe hao kwa ushawishi wao huo bado  alisema bado  anatafakari juu ya maombi hayo.

Japo  aliwataka  wanawake kwa mwaka  huu  kujitokeza kwa  wingi  kugombea nafasi za udiwani na ubunge katika wilaya  hiyo ya Mufindi ili  kuongeza chachu ya maendeleo na kuondoa  watu kujisahau katika nafasi zao.

Katika   kinyang’anyiro  cha kuomba  kuteuliwa  kugombea  ubunge ndani ya CCM mwaka 2010 jimbo la Mufindi  kusini  lilikuwa na wanachama 11 waliojitokeza  kuwania nafasi hiyo ambayo Bw Mendrady Kigola alishinda

Wengine waliojitokeza ni Thomas Bangu, Hassan Kalinga, aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo marehemu Benitho Malangalila, Faustine Mhapa, Michael Mlonganil, Mstapher Msovela, Mary Ngailo, Dk. Alex Sanga, Marehemu Sprian Tweve na Marcelina Mkini. Katika  kinyang’anyiro  hicho nafasi ya kwanza  ilichukuliwa na Kigola wakati nafasi ya  pili ilichukuliwa na marehemu Tweve na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Bi Mkini.