UTEUZI WA NAIBU GAVANA BENKI KUU YA TANZANIA

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Daktari Natu El-Maamry Mwamba kuwa Naibu Gavana wa Benki kuu ya Tanzania. Dkt. Mwamba anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt Enos Bukuku, ambaye aliteuliwa kuwa Naibu Katibu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwezi April, 2011. Uteuzi huu unaanza tarehe 13 Juni, 2011.

Kabla ya uteuzi huu, Dkt Natu El-Maamry Mwamba, alikuwa mhadhiri mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kitivo cha Uchumi.

Phillemon L. Luhanjo

Katibu Mkuu Kiongozi

Ikulu,

Dar Es Salaam

17 Juni, 2011