UNIC na Maadhimisho ya Siku ya Choo Duniani

Mwenyekiti wa Mtandao wa Asasi za Vijana Temeke (Temeke Youth Development Network -TEYODEN), Ismail Mnikite akitambulisha vijana waliohudhuria kutoka makundi mbalimbali.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Asasi za Vijana Temeke (Temeke Youth Development Network -TEYODEN), Ismail Mnikite akitambulisha vijana waliohudhuria kutoka makundi mbalimbali.


UNIC na Maadhimisho ya Siku ya Choo Duniani
Siku ya choo duniani ambayo huadhimishwa tarehe 19 Novemba. UNIC waliadhimisha siku hii kwa kuwakutanisha vijana walioko nje ya shule  tarehe 23 Desemba 2014 kwa lengo la kuwaelimisha na kuwahamasisha  utumiaji wa vyoo ili na wao waweze kuelimisha jamii zinazowazunguka juu ya umuhimu wa kuwa na vyoo.
Tukio hili liliwakutanisha vijana toka vikundi 5:   Azimio Youth Group, Makangarawe Youth Development Fund, Mashine Ya Maji Youth Development Centre,Temneke Youth Development Foundation na Tanzania Youth Development Society. Yafuatayo ni baadhi ya matukio katika picha.

TOILET DAY 2014 3 blog 1

Vijana wakiwa katika makundi kujadili na kuweka mikakati watakavyosaidia  jamii kuhusu utumiaji wa vyoo na usafi wa mazingira.

TOILOET DAY 2014 4 blog 1

Afisa Habari wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi.  Usia Nkhoma-Ledama akitoa mada kuhusu siku ya Choo duniani pamoja na umuhimu wa utumiaji vyoo, na kampeni maalumu ya uhamasishaji wa kuwa na vyoo.

TOILET DAY 2014 13 blog 2

Baada ya majadiliano, vijana wakiwasilisha maazimio na mikakati waliyoyakusudia kufanya ndani ya vikundi vyao katika jamii zinazowaunguka.
TOILET DAY 2014 19 blog 1