Rais Magufuli Kuzinduwa Rasmi Mabasi ya Mwendo Kasi Dar

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Joseph Magufuli, kesho tarehe 25 /01/2017 anatarajiwa kuzindua Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji wa Huduma ya Mabasi Yaendayo Haraka (Bus Rapid Transit – BRT) katika Kituo Kikuu cha Mabasi kilichopo Kariakoo eneo la Gerezani. Uzunduzi huo utahudhuriwa na Rais wa Benki ya Dunia, Kanda ya Afrika, Bw. …

Serikali Kupunguza Vizuizi Magari Yanayosafiri Nje ya Nchi

KATIBU Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Injinia Joseph Nyamhanga ametambulisha utaratibu mpya utakaotumika kupunguza vikwazo visivyo vya kiforodha ili kurahisisha biashara na usafirishaji kwa magari makubwa yanayosafiri kwenda nje ya nchi. Utaratibu huo unaotarajiwa kuanza Mei mwaka huu utawezesha magari yanayosafiri nje ya nchi kukagulia katika vituo visivyozidi vinne ili kupunguza muda wa safari kwa …

Eng. Edwin Ngonyani Azipa Changamoto Taasisi za Serikali

NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani, amezitaka taasisi zilizo chini ya Wizara yake kufanya kazi kwa uadilifu, bidii na kwa uharaka ili kuendana na kasi ya madiliko ya Serikali ya awamu ya Tano. Ameyasema hayo jijini Dar es salaam, wakati alipofanya ziara katika taasisi zilizo chini ya Wizara yake ikiwemo Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Wakala …

Je Huu ni Usafiri Kafiri Au..?

Pichani, ni wakazi wa jiji la Dar es Salaam kama walivyonaswa leo na mpiga picha wetu wakiwa kwenye heka heka za kuingia kwenye Daladala, ambalo lipo kimitego mitego kama picha inavyojionesha hapo juu. Picha hii inaonesha kidumu cha mafuta kikiwa kimefungwa kiaina (kienyeji) kutokea kwenye injini ndani ya basi la abiria. Hivi bahati mbaya ukija kutokea mlipuko ndani ya daladala …