Kipigo cha Taifa Stars: Mkwasa Awashukuru Watanzania

KOCHA Mkuu wa timuya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Boniface Mkwasa amewashukuru watanzania kwa kuwapa sapoti katika michezo miwili ya kuwania kufuzu kwa Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Urusi. Akiongea na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa mikutano wa TFF uliopo Karume, Mkwasa amesema pamoja na kupoteza nafasi ya kusonga mbele katika hatua ya makundi kuwania kufuzu …

Stars Kujaribu Bahati na Algeria, Kibadeni Awaita Kilimanjaro Stars

KIKOSI cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kinachodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, kitafanya mazoezi leo jioni saa 1 Algeria, sawa na saa 3 usiku kwa saa za Afrika Mashariki katika uwanja wa Mustapher Tchaker utakaotumika kwa mchezo wa kesho dhidi ya wenyeji Algeria. Stars inayonolewa na kocha mzalendo, Charles Boniface Mkwasa iliwasili salama jana jioni katika …

Taifa Stars Kutimkia Muscat Oman,TFF Yataja Waamuzi

TIMU ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajiwa kuondoka nchini siku ya jumamosi usiku kuelekea Muscat Oman, kucheza mchezo wa kirafiki kabla ya kuunganisha kuelekea Istambul Uturuki kwa kambi ya wiki moja. Taifa Stars imepata mwaliko wa kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Taifa ya Oman tarehe 24 Agosti, 2015 usiku, ambapo baada ya mchezo huo timu itasafiri kuelekea …

Mkwasa Atambulishwa Stars, Awaita Wachezaji 26

KATIBU Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa miguu Tanzania (TFF), Mwesigwa Selestine leo amemtambuisha kocha mpya wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Charles Boniface Mkwasa mbele ya waandishi wa habari. Akiongea na waandishi wa habari, Mwesigwa amewaomba wadau wa mpira wa miguu nchini kuwapa sapoti makocha hao wazawa wanaoanza kazi kesho kujiandaa na mchezo wa marudiano dhidi ya …

Taifa Stars Yawasili Borg El Arab Misri

MSAFARA wa timu ya Taifa ya Tanzania (taifa Stars) inayodhaminiwa na kampuni ya bia ya Kilimanjaro Premium Lager tayari umewasili salama katika eneo la Borg El Arab jijini Alexandria na kufikia katika hoteli ya Panacea tayari kwa mchezo wake wa kesho. Taifa Stars ambayo ilikuwa kambini nchini Ethiopia kwa takribani wiki moja, iliondoka jana usiku Addis Ababa na kuwasili uwanja …

Taifa Stars Yajifua Addis Ababa

TIMU ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhamini na kampuni ya bia ya Kilimanjaro, leo imeanza mazoezi katika uwanja wa Addis Ababa zamani ukifahamka kama (Haille Sellsie) uliopo jijini Addis Ababa kujiandaa na mchezo dhidi ya Misri utakaopigwa Juni 14, jijini Alexandria. Stars ambayo iliwasili jana jioni jijini Addis Ababa imefikia katika hoteli ya Debre Damo iliyopo eneo na 22 …