Serikali Yaahidi Kuisaidia NIDA Kufikia Malengo

NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima leo amefungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kilichofanyika katika Hoteli ya Kunduchi Beach ukumbi wa Kambarage, Dar-es-salaam na kuahidi serikali kuendelea kusaidia NIDA ili kufikia malengo ya serikali ya awamu ya Nne ya kila mtanzania kuwa amesajiliwa na kupata Kitambulisho chake. Akimkaribisha …

Serikali Kutumia Bil 55 Kusambaza Umeme Mbeya Vijijini

  WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema Serikali itatumia shilingi bilioni 55 kuvipatia umeme vijiji 244 vya mkoa wa Mbeya kupitia Miradi ya Umeme Vijijini (REA). Ametoa kauli hiyo Machi 2, 2015 wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Mbeya waliofika kusikiliza majumuisho ya ziara yake ya siku saba kwenye mkoa huo. Mkutano huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Mkapa, jijini …

Wanasiasa Tanzania Wahusishwa na Mauaji ya Albino!

Katika makala iliyopewa jina la “Love in a Time of Fear: Albino Women’s Stories From Tanzania”, iliyorushwa kwenye gazeti la intaneti la Huffington Post (tarehe 25/10/2013 na kuhuwishwa tena tarehe 23/01/2014) kutoka Marekani, ililbaini kwamba wanasiasa wa Tanzania wanahusishwa na mauaji ya albino, na kipindi cha uchaguzi ndio kipindi hatari kwa maisha ya albino nchini. Kuhusishwa huko kwa wanasiasa wa Tanzania, …

Mauaji Haya ya Albino Mpaka Lini?

      Na Evarist Chahali 25/2/2015   “Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wote, Nchi yangu Tanzania, jina lako ni tamu sana Nilalapo nakuwaza wewe, niamkapo ni heri mama wee. Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wote.” Huu ni ubeti wa wimbo maarufu ambao ‘zamani hizo’ tulipouimba tulijisikia ‘raha’ flani kuhusu nchi yetu. Tulikuwa na kila sababu za kuipenda Tanzania kiasi …

Serikali Kuajiri Walimu Zaidi ya 35,000

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema Serikali imepanga kuajiri walimu zaidi ya 35,000 kwa ajili ya shule za sekondari ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa walimu nchini. Ametoa kauli hiyo jana Februari 19, 2015 wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa kata ya Kiwere, mara baada ya kukagua ujenzi wa maabara na kuzindua nyumba nne za walimu kwenye shule ya …

PAC Yaishauri Serikali Namna ya Kuinusuru TTCL

KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imetoa mapendekezo ya kuinusuru Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kutokana na hali mbaya ya kampuni hiyo kifedha kwa sasa ambapo inaendeshwa kwa hasara huku ikiwa na madeni makubwa. PAC imetoa mapendekezo hayo katika taarifa yao kwa bunge ya mwaka juu ya ukaguzi wa hesabu za Serikali kwa mashirika ya umma iliyotolewa Januari …