JK: Salama ya Burundi ni Kuheshimu Katiba na Sheria

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete na Mwenyekiti wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), amewashauri viongozi na wananchi wa Burundi kufanya mambo manne muhimu ili kutuliza hali ya sasa ya kisiasa katika nchi hiyo na hivyo kuepusha ukosefu wa utulivu wa kisiasa na hata kuzuka kwa machafuko. Rais Kikwete …

Ipitisheni Katiba Inayopendekezwa – Mama Kikwete

Na Anna Nkinda – Maelezo, Lindi MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia wilaya ya Lindi mjini Mama Salma Kikwete amewaomba wananchi kuipigia kura ya ndiyo katiba inayopendekezwa kwa kuwa ni bora na imezingatia mahitaji ya makundi yote ya jamii. Mama Kikwete ambaye ni Mke wa Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ametoa ombi hilo …

FemAct Watoa Tamko Kuhusiana na Katiba Pendekezwa

TAMKO LA FEMACT KUHUSU VURUGU ZILIZOTOKEA KATIKA MDAHALO KUHUSU KATIBA PENDEKEZWA KATIKA HOTEL YA BLUE PERL UBUNGO DAR ES SALAAM TAREHE 2 NOVEMBER 2014. Sisi Mashirika yapatayo 50 yanayotetea Usawa wa Kijinsia, Haki za Binadamu, Demokrasia, Utawala bora, Maendeleo na Ukombozi wa Mwanamke Kimapinduzi ( FemAct ) tumekuwa tukifuatilia kwa karibu mchakato wa katiba unavyokwenda tangu ulipoanza. Pamoja na changamoto …

Wananchi Bukina Faso Waandamana Kumpinga Rais

KUMETOKEA vurugu kubwa baina ya maelfu ya waandamanaji na maofisa wa polisi katika Mji Mkuu wa Burkina Faso, Ougadougou wakati maelfu ya raia wa nchi hiyo walipokuwa wakihudhuria mkutano kupinga marekebisho ya Katiba itakayomruhusu rais wa nchi hiyo, Blaise Compaore kuongoza nchi kwa kipindi kingine cha miaka mitano. Maofisa wa usalama walitumia mabomu ya kutoa machozi dhidi ya wanadamanaji hao …

JK Aanza Kuinadi Katiba Inayopendekezwa Mwanza

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete amewashangaa watu wanaodai kuwa Katiba Inayopendekezwa ni mbaya, akiuliza kuwa kama Katiba hiyo ni mbaya basi hiyo nzuri ikoje? Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa Katiba inayojali makundi yote ndani ya jamii, kama ilivyo Katiba Inayopendekezwa, kamwe haiwezi kuwa Katiba mbaya. Rais Kikwete ameyasema hayo nyakati tofauti, Oktoba 10, 2014, wakati alipozungumza …