JK Ateuwa Wabunge Wawili Wapya

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, amewateua wabunge wawili (2) wapya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Walioteuliwa ni Dk. Grace Khwaya Puja na Bwana Innocent Sebba. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari kutoka ikulu leo, Rais amefanya uteuzi huu kwa mamlaka aliyopewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, …