Serikali Haina Nguvu Kuzungumzia Uraia Pacha – Rais Kikwete

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibonyeza kitufe kuzindua tovuti rasmi ya Diaspora wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa Diaspora katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam Agosti 14, 2014. Pamoja naye ni Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda, Mwenyekiti wa Taasisi ya Diaspora Bw. Emmanuel Mwachullah (wa pili kulia), Mwana-Diaspora Dennis Londa (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Diaspora Bi. Rose Jairo. PICHA NA IKULU.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibonyeza kitufe kuzindua tovuti rasmi ya Diaspora wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa Diaspora katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam Agosti 14, 2014. Pamoja naye ni Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda, Mwenyekiti wa Taasisi ya Diaspora Bw. Emmanuel Mwachullah (wa pili kulia), Mwana-Diaspora Dennis Londa (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Diaspora Bi. Rose Jairo. PICHA NA IKULU.

Rais Jakaya Kikwete akifungua mkutano wa kwanza wa Diaspora katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam Agosti 14, 2014. PICHA NA IKULU.

Rais Jakaya Kikwete akifungua mkutano wa kwanza wa Diaspora katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam Agosti 14, 2014. PICHA NA IKULU.

Rais Jakaya Kikwete akifungua mkutano wa kwanza wa Diaspora katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam Agosti 14, 2014. PICHA NA IKULU.

Rais Jakaya Kikwete akifungua mkutano wa kwanza wa Diaspora katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam Agosti 14, 2014. PICHA NA IKULU.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mkrisho Kikwete akiingia ukumbini wakati wa kongamano la Watanzania waishio Ughaibuni lililofanyika kwa mara ya kwanza nchini Jijini Dar es Salaam. Nyuma yake ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizendo Pinda (mwenye koti la Bluu). Picha na Hassan Silayo-Maelezo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mkrisho Kikwete akiingia ukumbini wakati wa kongamano la Watanzania waishio Ughaibuni lililofanyika kwa mara ya kwanza nchini Jijini Dar es Salaam. Nyuma yake ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizendo Pinda (mwenye koti la Bluu). Picha na Hassan Silayo-Maelezo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizendo Pinda akiwaeleza jambo Watanzania waishio Ughaibuni wakati wa kongamano la Watanzania waishio ughaibuni lililofanyika kwa mara ya kwanza nchini Jijini Dar es Salaam. Picha na Hassan Silayo-Maelezo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizendo Pinda akiwaeleza jambo Watanzania waishio Ughaibuni wakati wa kongamano la Watanzania waishio ughaibuni lililofanyika kwa mara ya kwanza nchini Jijini Dar es Salaam. Picha na Hassan Silayo-Maelezo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akiangalia tovuti ya Umoja wa Watanzania waishio nje ya baada ya kuizindua tovuti hiyo jijini Dar es Salaam. Picha na Hassan Silayo-Maelezo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akiangalia tovuti ya Umoja wa Watanzania waishio nje ya baada ya kuizindua tovuti hiyo jijini Dar es Salaam. Picha na Hassan Silayo-Maelezo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mkrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na watanzania waishio Ughaibuni wakati wa kongamano la Watanzania waishio ughaibuni lililofanyika kwa mara ya kwanza nchini, Jijini Dar es Salaam. Picha na Hassan Silayo-Maelezo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mkrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na watanzania waishio Ughaibuni wakati wa kongamano la Watanzania waishio ughaibuni lililofanyika kwa mara ya kwanza nchini, Jijini Dar es Salaam. Picha na Hassan Silayo-Maelezo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mkrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na watanzania waishio Ughaibuni wakati wa kongamano la Watanzania waishio ughaibuni lililofanyika kwa mara ya kwanza nchini, Jijini Dar es Salaam. Picha na Hassan Silayo-Maelezo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mkrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na watanzania waishio Ughaibuni wakati wa kongamano la Watanzania waishio ughaibuni lililofanyika kwa mara ya kwanza nchini, Jijini Dar es Salaam. Picha na Hassan Silayo-Maelezo.

Na Joseph Ishengoma

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete amesema hana mamlaka ya amri kuzungumzia uraia pacha kwasababu suala hilo ni la kikatiba. Rais Kikwete alisema hayo katika Kongamano la Kwanza la Diaspora lililofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Diaspora ni lugha inayotumika kuwatambulisha Watanzania walioko nje ya nchi wanaojiendeleza kwa njia mbalimbali ikiwemo elimu. Kongamano hilo la siku mbili lenye lengo la kuelimishana, kubadilishana mawazo na kujadili fursa za uwekezaji, linaudhuriwa na wajumbe kutoka nchi 17 duniani.

“Serikali imelisikia suala la uraia pacha, lakini ni la kikatiba sio la Rais. Katiba ndio sheria mama sisi hatuna mamlaka ya amri kulizungumzia.”

Kwa mujibu wa Rais, watanzania waliowengi uraia pacha hauwakeleketi, hivyo diaspora wanaoishi nje ndio wanaostahili kulisukuma, lakini kwa sasa sauti yao bado haijasikika sana, badala ya kulizungumzia kwa nguvu, wanatumia muda mwingi kuzungumzia siasa za mitaani kwenye mitandao ya kijamii pindi wanapopata nafasi.

“Sauti yenu haijasikika sana, badala yake mnatumia muda mwingi kuzungumzia siasa za mitaani. Suala la uraia pacha liko mikononi mwa Bunge Maalum la Katiba. Kama katiba haijasema nyinyi ni rais, sheria ikitungwa haiwezi kuwapa uraia,” amesema.

Kwa mujibu wa Rais, rasmu ya Katiba iliyopo inazungumzia hadhi ya Watanzania walioko nje sio uraia. “Mnachoweza kufanya ni kushawishi wabunge wa Bunge Maalum la Katiba kukubali uraia pacha kuwa ndani ya katiba na hili sio jambo haramu, zungumzeni nao serikali haina tatizo nalo iwapo Katiba itawatambua.”

Pamoja na uraia pacha, Rais amewaomba wanadiaspora kuzingatia uwekezaji ndani ya nchi ili kuleta maendeleo ya kiuchumi, kutafuta masoko ya bidhaa ya bidhaa za Tanzania nje ya nchi, kuunda umoja utakaowaunganisha na kutumia teknolojia na maalifa wanayopata nje kuendeleza taifa lao.

Kauli mbiu ya kongamano hilo ni, “Nyumbani ni Nyumbani.” Awali Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Mizengo kayanza Pinda ametaka mkutano huo kusaidia kukata kiu ya Watanzania kupata majibu ya mambo ambayo wamekuwa wakiulizia pindi wanapokutana na viongozi mbalimbali wa nchi nje ya Tanzania.