Samsung Wazinduwa Simu ya Ajabu Aina ya 4G LTE

Samsung Wazinduwa Simu ya Ajabu Aina ya 4G LTESamsung Wazinduwa Simu ya Ajabu Aina ya 4G LTE

Samsung Wazinduwa Simu ya Ajabu Aina ya 4G LTE

Samsung Wazinduwa Simu ya Ajabu Aina ya 4G LTE
Samsung Wazinduwa Simu ya Ajabu Aina ya 4G LTE

NGULI wa vifaa vya umeme Samsung imeendelea na juhudi za kuimarika katika nafasi ya kwanza kwa uzinduzi wa simu zake mpya na za kushangaza za 4G LTE zilizo pewa jina la ‘Muvika’. Uzinduzi huu wa mara ya kwanza na wa aina yake nchini kwa upande wa simu za mkononi zenye teknolojia ya aina hii ulifanyika Hoteli ya Bay Leaf Arusha. Pamoja na utambulisho huo tukio lilikuwa kama jukwaa la usimamizi wa wazalishaji simu kukutana na wafanyabiashara wa hapa nyumbani, mawakala na wadau wengine muhimu.

Soko la simu za mkononi Arusha ni moja kati ya yale ambayo kampuni inayatazama kama fursa ya pekee na ilikuwa sababu ya kuchagua Arusha kwa uzinduzi wa 4G LTE mbali na Dar es Salaam. Kutoka a ukuaji wa uchumi mkoani hapa na sekta kama za utalii na madini zinazosaidia katika maendeleo ya kiuchumi makampuni mengi kama Samsung yanakuja kwa kasi kuhakikisha huduma/bidhaa zao haziko mbali na wateja wao muhimu.

Uzinduzi ulifanyika mbele ya wageni waalikwa kutoka mkoani hapo kukiwa na burudani ya moja kwa moja kutoka kwa ‘msanii maarufu’ na balozi wa kampuni ya vifaa vya umeme ya Samsung Tanzania Vanessa Mdee.
Akiongea wakati wa sherehe za uzinduzi Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya vifaa vya umeme ya Samsung Tanzania, Bw Hyeongjun Seo, aliongelea mahusiano mazuri yaliyopo katiya kampuni na watu wa Arusha na umuhimu wa kuzingatia huduma bora na bidhaa inayoendana na Samsung.

Alisema “Arusha ni mkoa muhimu kibiashara na hatuangalii tu kuendelea kutoa ubora wa uzoefu wetu kwa wateja lakini pia kuwapa bidhaa za kisasa na za kibunifu zinazoendana na soko la kimataifa.” Maoni ya Mkurugenzi mtendaji yaliungwa mkono na Sylvester Manyara, Mkuu wa Mauzo na Usambazaji Samsung Electronics Tanzania akisema “Leo tunazindua teknolojia hii katika uwepo wa mawakala na wasambazaji wetu, tumechagua Arusha ikiwakilisha nia ya kuendelea kukua ambako ni sehemu ya utamaduni wa Samsung.”

‘Muvika’ ni neno lisilo rasmi linalo jaribu kuelezea uwezo wa simu hii na wepesi wake katika mtandao unaokuja na 4G LTE unaowawezesha watumiaji kupata hadi filamu kwa kasi ya kushangaza. 4G LTE (Mabadiliko ya Kudumu ya Kizazi cha Nne) ni simu yenye teknolojia ya kisasa katika mtandao inayoipeleka Dunia kwa kasi.

Kwa mahitaji yanayo ongezeka ya simu za kisasa zenye uwezo kama huu Samsung Tanzania wanahakikisha kuwa mahitaji ya wateja wao yanafikiwa. Akiwa kama balozi wa bidhaa za Samsung Tanzania, Bi. Vanessa Mdee atakuwa kama uso wa simu zitakazo tolewa chini ya mwamvuli wa Muvika. Akichangia juu ya wajibu wake Vanessa alisema “Huu ni ukurasa mwingine mzuri zaidi tunao ufungua na Samsung tangu tulipoianza safari yetu pamoja na kama mzaliwa wa Arusha nafurahi kupata fursa hii kuwa mstari wa mbele wa mabadiliko ya teknolojia ambayo Samsung wanaanzisha.”