Rais Zuma Awatembelea Raia wa Kigeni Wanaoshambuliwa Afrika Kusini

Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma.

Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma.


RAIS Jacob Zuma amewatembelea watu walioathirika na ghasia hizo, mauwaji pamoja na kuibwa kwa mali zao huku akiahidi kukabiliana vilivyo na wimbi la mashambulio hayo.

Bwana Zuma alifutilia mbali ziara yake nchini Indonesia, ili kukabiliana na vurumai hizo zilizoanza majuma mawili yaliyopita. Amesema kuwa ghasia hizo ni kinyume na maadili ya taifa la Afrika kusini. Maofisa zaidi wa polisi wametumwa katika maeneo yenye mashambulio dhidi ya raia wa kigeni nchini Afrika Kusini.

Yamkini watu sita wameuawa na makundi yenye silaha, ambayo yanawalaumu wahamiaji wa kiafrika kwa kuchukua kazi zao nchini Afrika Kusini. Yamkini watu sita wameuawa na makundi yenye silaha, ambayo yanawalaumu wahamiaji wa kiafrika kwa kuchukua kazi zao nchini Afrika Kusini.

Nchini Harare Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, alilaani ghasia hizo. Ghasia hizo zilianza baada ya mfalme mmoja wa Kizulu, Goodwill Zwelethini, kusema kuwa raia wa kigeni sharti waondoke Afrika Kusini.

Akiongea katika kambi hiyo iliyoko mjini Durban kiongozi mkuu wa jimbo la Gauteng, David Makhura, anasema kuwa uhasama na ghasia hizo zinazoshuhudiwa, hauandamani na uhuru wa miaka mingi ambayo Afrika Kusini ilipigania.

-BBC