Rais Kikwete haudhuria mkutano wa biashara Malaysia

President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete speaks during the panel discussion on Innovative Financing for Transformation during the ongoing Langkawi International Dialogue (LID) 2011 held at Putrajaya, Malaysia this morning. Other panelists from left are Namibia's Deputy Prime Minister Marco Hausiku and second left is the Malaysia's Central Bank Governor Dr. Zeti Akhtar Aziz. The Langkawi International Dialogue is aimed at spurring more business and trade between Malaysia and the African continent. (Photos by Freddy Maro)

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwasili mjini Kuala Lumpur, Malaysia leo, Juni 19, 2011 kuungana na viongozi wenzake kutoka nchi mbalimbali katika mkutano wa mwaka huu wa Smart Patrnership Dialogue.
Mkutano huo ambao umekuwa unafanyika kila mwaka kwa miaka 16 sasa tokea mwaka 1995, unatokana na uamuzi wa wakuu wa nchi za Jumuia ya Madola uliofanyika Cyprus mwaka 1993 na kuzinduliwa rasmi katika mkutano wa wakuu, uliofanyika Auckland, New Zealand mwaka 1995.
Mkutano huo huzungumzia masuala mbali mbali ya maendeleo na hasa umuhimu wa uhusiano mzuri kati ya Serikali, sekta ya umma na sekta binafsi katika kuleta maendeleo. Mkutano wa mwaka huu umepangwa kufanyika katika Kituo cha Mikutano ya Kimataifa cha Putrajaya (PICC) kilichoko katika mji mpya wa shughuli za Serikali ya Malaysia ulioko Patrajaya, nje kidogo ya mji wa asili wa Kuala Lumpur.
Nchi ya Malaysia imewaalika wakuu 25 wa nchi mbali mbali duniani kushiriki katika mkutano huo japokuwa haitarajiwi wote kushiriki mkutano huo. Kutoka Afrika amealikwa Rais Kikwete, Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, Rais Omar El Bashir wa Sudan na Waziri Mkuu wa Lesotho.
Rais Kikwete atanawasili Malaysia kuhudhuria mkutano huo akitokea Shelisheli ambako alikuwa mgeni rasmi katika sherehe za Siku ya Taifa la Shelisheli.
Mbali na kuhudhuria mkutano huo atazungumza kwenye kikao cha ufunguzi na pia kwenye kikao kitakachozungumzia namna mbadala na za ubunifu zaidi za kupata fedha kwa ajili ya maendeleo, Rais Kikwete pia atakuwa na shughuli nyingine muhimu za kikazi.
Miongoni mwa shughuli hizo ni Rais Kikwete kukutana kwa mazungumzo na Waziri Mkuu wa Malaysia, Dato’ Sri Mohammed Tun Abdul Razak, kukutana kwa mazungumzo na aliyekuwa waziri mkuu wa Malaysia, Mheshimiwa Tun Dkt. Mahathir Mohamad, Rais wa Heshima wa Taasisi ya Uongozi ya Perdana Leadership Foundation.
Rais Kikwete pia atakutana na kula chakula cha usiku na wenyeviti, marais na watendaji wakuu wa makampuni makubwa ya Malaysia wakiongozwa na Mheshimiwa Mahathir Mohamed.