Ofisi ya TAMISEMI Waongoza kwa Rushwa Mwanza

Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rusha mkoani Mwanza akizungumza na wanahabari hawapo pichani.

Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rusha mkoani Mwanza akizungumza na wanahabari hawapo pichani.

MKUU wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rusha mkoani Mwanza Mhandisi Ernest Makale, leo ametoa taarifa ya Utendaji kazi wa taasisi hiyo mbele ya Wanahabari katika kipindi cha robo mwaka (Januari hadi Machi) mwaka huu.
Katika taarifa hiyo, Mhandisi Makale amebainisha kuwa Takukuru imepokea jumla ya malalamiko 45 yanayohusiana na vitendo vya rushwa kutoka kwa wananchi ambapo katika malalamiko hayo, 27 yameelekezwa kwa watumishi wa idara za Serikali za Mitaa TAMISEMI hiyo ikiwa ni sawa na asilimia 60. Kati ya malalamiko hayo 27, malalamiko 13 yameelekezwa katika idara ya ardhi.