Mwanamuziki Chill Challa wa Skylight Band Azikwa

Watoto wa kiume wa marehemu Chill Challa wakiweka shada la maua kwenye kaburi la Baba yao.

Watoto wa kiume wa marehemu Chill Challa wakiweka shada la maua kwenye kaburi la Baba yao.

Baadhi ya waombolezaji wakibadilishana mawazo katikati ni mwanamuziki wa Skylight band Joniko Flower

Waombolezaji wakiendelea kubadilishana mawazo wakati wakisubili mwili wa marehemu Kufika.

Mkurugenzi wa Skylight Band akijadili jambo na Aneth Kushaba ili kuweka mambo sawa kabla ya mwili wa marehemu kuwasili.

Gari iliyobeba mwili wa marehemu Chill Challa likiwasili nyumbani kwa marehemu.

Ndugu na jamaa wakishusha mwili wa marehemu Chili Challa.

Mwili wa marehemu ukishushwa kwa ajili ya ibada

Mchungaji wa kanisa alipokuwa Anasali marehemu akiongoza ibada ya kumuombea Marehemu Ayoub Songoro maaru Chill challa aliyekuwa mwanamuziki na mpiga Gita wa Skylight Band.

Misa ya kumuombea marehemu akiendelea nyumbani kwake Mwananyamala

Mke wa marehemu akiwa na majonzi.

Meneja wa bendi ya Skylight Aneth Kushaba akiaga mwili wa marehemu.

Waombolezaji wakiaga mwili wa marehemu.

Mkurugenzi wa Skylight Band akiaga mwili wa marehemu.

Watoto wa marehemu wakiwa na majonzi ya kuondokewa na baba yao kipenzi.

Kaka wa marehemu akiaga mwili wa mdogo wake kwa huzuni kubwa

Mwili wa marehemu ukipandishwa kwenye gari Tayari kwenda kuzikwa baada ya ibada ya kumuombea

Msafara ukielekea makaburi ya Mwananyamala kwa kopa

Mwili wa marehemu ukishushwa kaburini tayari kwa kuzikwa

 

Wanamuziki wenzake na marehemu wakifuatilia mazishi ya mwenzao

Mchungaji akisoma neno

Mchungaji akirusha udongo kuonyesha ishara ya kuaza maziko

Mke wa marehemu akirusha udongo ndani ya kaburini

Watoto wa kiume wa marehemu wakirusha udongo kaburini kumzika baba yao

Kaka wa marehemu akiwa  akimzika mdogo wake

Mkurugenzi wa Skylight Band akirusha udongo kumzika msanii wake

Aneth kushaba akirusha udongo kumzika marehemu

Waombolezaji wakiwa wanafuatilia maziko kwa huzuni kubwa

Mchungaji akiweka msalaba kwenye kaburi la marehemu

Mke wa marehemu akiweka shada la maua kwenye kaburi

Ndugu wa Marehemu wakiweka Shada la maua

Mpiga Gita mahiri wa bendi ya Skylight Chill challa amezikwa jana kwenye makaburi ya Mwananyamala kwa kopa na mamia ya watu na wanamuziki wenzie. Marehemu Chill challa alifariki Tar 17-04-2014 hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Chanzo cha kifo cha marehemu ni shinikizo la damu ambapo kabla ya kifo chake alikuwa katika afya njema, lakini Usiku wa Tar 16 marehemu alidondoka gafla bafuni na ndipo alipkimbizwa hospitalini.

Madaktari walijitaidi kwa kila hali na mali kuokoa uhai wa marehemu lakini ilishindikana kutokana na shinikzo la damu kuwa kubwa sana na ndipo Chill challa akafariki dunia, Marehemu Chill challa ameacha Mke na watoto wawili, Marehemu alikuwa ni mpiga gita mzoefu na mahiri ambaye amepitia karibu bendi zote kubwa na kongwe nchini kama Akudo, Fm academia na zingine nyingi. Uongozi mzima wa Skylight band unawashukuru wale wote waliojitoa kwenye msiba huu na Mungu awabariki. PICHA ZOTE NA DJ SEK BLOG