Mmiliki CCJ amlipua Mpendazoe

 

Na Said Mwishehe

MMILIKI wa Chama Cha Jamii(CCJ) Richard Kiyabo ameamua

kuvunja ukimya na kutaja majina ya waalinzishi wa chama

hicho huku akitumia nafasi hiyo kumshambulia kada wa

Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Fred

Mpendazoe kuwa anatabia ya kukurupuka na kumtaka aache

siasa za udaku.

Amesisitiza kitendo cha Mpandazoe kumtaja Katibu wa

Itikadi na Uenezi Nape Nnauye, Waziri wa Ushirikiano wa

Afrika Mashariki Samuel Sitta na Naibu Waziri wa Ujenzi

Dk. Harrison Mwakyembe kuwa ni waanzilishi wa CCJ ni

jambo linaloshangaza na kwamba Mpandazoe amejivunjia

heshima aliyokuwa nayo kwa Watanzania.

Pia CCM Mkoa wa Dar es Salaam,imeitak CHADEMA nayo

kujivua gamba la ukabila kutokana na kuwa na wabunge

wengi wa viti maalumu kutoka Kanda ya Kaskazini huku pia

wakitakiwa kujibu hoja za Nape na hasa kuhusu mshahara

wa sh.milioni 7.5 anazolipwa Katibu Mkuu willibrod Slaa

wakati.

Akizungumza Dar es Salaam jana, kuhusu waanzilishi na

wamiliki wa CCJ, mmiliki huyo ambaye pia ndio alikuwa

Mwenyekiti wa CCJ, Kiyabo alisema kuwa chama hicho

kilianzishwa na yeye na Katibu Mkuu wake Renatus Muabhi

na ndio walikuwa wanahusika na kila kitu kuhusu

uuanzishwaji wa CCJ na hakuna mwanasiasa mwengine zaidi

yao.

Alisema hata katika usajili wa chama hicho kwa Msajili

wa Vyama vya Siasa John Tendwa majina yaliyopo ni ya

watu wawili ambapo ni yeye na Muabhi na kwamba hakuna

jina la Sitt, Mwakyembe wala Nape kama anavyodai

Mpandazoe ambaye naye alijuunga baada ya chama hicho

kuanza.

“Wakati CCJ inaanza mimi ndio nilikuwa nafanya kila kitu

kwa kushirikiana na Muabhi ambaye ndio alikuwa Katibu

Mkuu wa CCJ. Wakati tunaanzisha CCJ nachokumbuka Nape

alikuwa masomoni India. Hivyo miongoni mwa waliojiunga

nasi ni Mpandazoe ambapo baada ya kujiunga alitaka awe

mwenyekiti tukamkatilia na kwa kumpa heshima akawa

msemaji wa chama,” alisema Kiyabo.

Alifafanua kuwa wakati CCJ inaanza haikuwahi kuwa na

Sitta, Mwakyembe wala Sitta hivyo anachokisema Mpandazoe

ni kutoa kauli za uzhushi na zilijaa uongo mtupu na

kukurupuka ni kawaida yake ndio maana aliweza kukuruka

kwa kumkimbia mkewe Rose na watoto wake na kisha

kukimbia CCM na jimbo lake la Kishapu.

“Mpendazoe anadai kuwa waheshimiwa hao walikuwa ni

waanzilishi wa CCJ, hoja hiyo ni ya utata mkubwa.Swali

la kuuliza Mpendazoe wakati anaondoka CCM na kujiunga

CCJ alipokelewa na nani kati ya haoo anaowataja?

Walikuwa na nyadhifa zipi na namba za kadi zao za

uanachama.Je amesahau kuwa yeye alinukuliwa na vyombo

vya habari akimkaribisha Sitta CCJ,” alisema Kiyabo.

Aliongeza kuwa Mpandazoe hana hoja ya msingi kuhusu

kauli ambazo anazitoa na waanzilishi wa CCJ ambayo hivi

sasa ni marehemu kwa kuwa ilishakufa muda mrefu na

kuanzishwa kwa CCK na kumfananisha Mpendazoe kuwa hana

tofauti na mwanasiasa mdakuwa wa kisiasa yeye na chama

chake na kwamba wasidhani hiyo ni sera itakayowafikisha

Ikulu.

Kiyabo alisema kuwa anamshauri Mpendazoe na wenzake wa

CHADEMA waache siasa alizoziita za udaku na kwamba

Watanzania wanataka kusikia sera za chama husika na siyo

udaku. Wakiendelea na udaku wa kuwatuhumu watu kila

kukicha, mwisho wataanza kuamini pengine ndio sera yao.

Pia alisema hivi sasa CHADEMA inaonesha nguvu ya umma si

kura tena bali maandamano na vurugu zenye lengo la

kuitoa Serikali madarakani.Wao wanajiita chama cha

demokrasia na maendeleo lakini ajabu wanayoyafanya si ya

kidemokrasia bali ni chama cha maandamano na vurugu.