Matukio Mbalimbali ya Upigaji Kura Uchaguzi Mkuu…!

Mkazi wa Njia ya Ng'ombe Mbagala Kuu, Sarah Simba akipiga kura katika kituo cha Shimbwe Dar es Salaam leo asubuhi kwa ajili ya kuwachagua viongozi wake, Rais, Mbunge na Diwani.

Mkazi wa Njia ya Ng’ombe Mbagala Kuu, Sarah Simba akipiga kura katika kituo cha Shimbwe Dar es Salaam leo asubuhi kwa ajili ya kuwachagua viongozi wake, Rais, Mbiunge na Diwani.

 Rukia Omari (kushoto), akimsaidia kupiga kura jamaa yake Mwanaharusi Mohamed ambaye ni mlemavu wa macho wakati wa kupiga kura katika kituo cha Mbagala Misheni Dar es Salaam leo asubuhi.
Wananchi wakiwa wamejipanga foleni kwa ajili ya kupiga kura katika Kituo cha Mtoni Kijichi Stendi Dar es Salaam leo asubuhi.
 Wananchi wakisubiri kupiga kura katika kituo cha Shimbwe Mbagala Kuu.
 Hapa wakihakiki majina yao.
 Wananchi wakiwa katika foleni ya kwenda kupiga kura katika kituo cha Ofisi ya Mtendaji Kata ya Mbagala Kuu.
 Wananchi wakiwa katika foleni ya kupiga kura katika kituo cha Shule ya Msingi Bwawani Mtoni Kijichi leo asubuhi.
 Wananchi wakiwa wamejipanga foleni kwa ajili ya kupiga kura katika Kituo cha Mtoni Kijichi Stendi Dar es Salaam leo asubuhi.
 Wasimamizi wa uchaguzi katika kituo cha Mbagala Misheni wakiwa kazini.
Msimamizi wa uchaguzi Mkuu katika kituo cha Mbagala Misheni, Yona Komba (kulia), akimpaka winoMwanaharusi Mohamed ambaye ni mlemavu wa macho baada ya kumaliza kupiga kura katika kituo hicho Dar es Salaam  leo asubuhi. Kushoto ni binti aliyemuomba amsaidie kupiga kura  Rukia Said.
 

Wasimamizi wa uchaguzi wakiendelea kuwahudumia wananchi waliofika katika kituo cha Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Kijitonyama leo jijini Dar kwa ajili ya kupiga kura. Picha na Geofrey Adroph wa Pamoja Blog

Mmoja wa wazee akisaidiwa na mtu wake wa karibu ili kupiga kura katika kituo cha Chuo cha Ustawi wa Jamii  jijini Dar le0.
Mlemavu akisaidiwa na mtu wa karibu alipofika katika kituo cha Kenton kwa ajili ya kupiga kura
Mmoja wa wananchi akiwa kwenye sehemu ya kupigia kura katika kituo cha kupigia kura kwenye Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Kijitonyama leo jijini Dar.
Wananchi wakihakiki majina yao katika kituo cha Shule ya Sinza  Mapambano jijini Dar leo.
 Wananchi  wakibadishana mawazo walipokuwa kwenye foleni wakisubiri kupiga kura katika kituo cha Shule ya Sinza  Mapambano jijini Dar leo.
 Wananchi wakihakiki majina yao katika kituo cha Shule Kenton Mwenge jijini Dar leo
 Wananchi wakisubiri kupiga kura katika kituo cha cha Shule ya Sinza Mapambano jijini Dar leo.
  
 
   Wananchi wakiwa wamejipanga foleni kwa ajili ya kupiga kura katika kituo cha Shule ya Sinza  Mapambano jijini Dar leo.
 Wananchi wakisubiri kupiga kura katika kituo cha Shule Kenton Mwenge jijini Dar leo

   Wananchi wakisubiri kupiga kura katika kituo cha Chuo cha Ustawi wa Jamii  jijini Dar leo
Umati mkubwa ukiwa kwenye foleni katika katika kituo cha kupigia kura kwenye Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Kijitonyama leo jijini Dar.
 Wakazi wa Segerea wakiwa katika foleni kwaajili ya kuendelea na zoezi la kupiga kura katika kituo cha Magereza Segerea muda huu huku hali ya usalama ikiwa shwari kabisa
 Foleni ikiwa bado ndefu huku mwamko ukiwa mkubwa kwa rika zote kuanzia vijana na wakina mama na baba zoezi linaendelea vizuri mpaka sasa
 Blogger Josephat Lukaza akiwa katika  foleni ya kupiga kura katika kituo changu cha Magereza segerea kwaajili ya kupiga kura kumchagua kiongozi atakayenifaa
Picha zote na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog
 Wakazi wa Segerea ambao wamjiandikisha katika kituo cha Segerea Magereza wakiwa wamejitokeza kwa wingi muda huu katika kituo hiko kwaajili ya kushiriki zoezi la kupiga kura kuwachagua viongozi mbalimbali kuanzia Rais, wabunge na Madiwani. Hali ni shwari hakuna vurugu wala viashiria vyovyote vile vya vurugu japokuwa kuna changamoto za hapa na pale ambapo mkazi mmoja ameambiwa na msimamizi wa uchaguzi kuwa hawezi kupiga kura kutokana na namba ya Kitambulisho chake cha kupigia Kura kutofautiana tarakimu moja tu na Namba ya kitambulisho iliyoandikwa katika karatasi la majina ya kuhakiki. Mkazi huyo ambaye hakupenda jina lake litajwe amesema kuwa anasubiri Mkuu wa kituo cha Uchaguzi Segerea Magereza kuweza kuongea nae na Kutatua swala hilo endapo ataruhusiwa basi atapiga kura na asiporuhusiwa basi hatopiga kura
Wakazi wa Segerea wakiwa kwenye foleni kusubiri kupiga kura
Baadhi ya wakazi wa segerea wakiwa katika foleni tayari kwa kupiga kura.Picha Na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog

Endelea kuwa nasi hapa tutakuletea kila kinachojiri kwenye vituo vilivyo karibu yetu
Ni katika Vituo mbalimbali Jijini Mwanza ambapo zoezi la Upigaji Kura limeenda vyema huku likitawaliwa na utulivu katika vituo mbalimbali vya kupigia kura.
Na:George GB Pazzo
Katika Mitaa mbalimbali ya Jiji la Mwanza hakukuwa na foleni za Magari kama ilivyozoeleka na hata shughuli nyingi zilisimama ili kupisha zoezi hili na muda si mrefu mbivu na mbichi zitaanza kujulikana hivyo ni vyema pande zote zikawa tayari kuyapokea matokeo kwani kwenye uchaguzi kuna kushinda na kushinwa.
Zoezi la upigaji kura limetawaliwa na utulivu wa hali ya juu katika vituo mbalimbali huku hamu ya kila mmoja kushiriki zoezi hilo ikiwa ni kubwa pia
Wakazi wa Jiji la Mwanza wakiendelea na zoezi la kupiga kura
Kulia ni Makoye Magige ambae ni Msimamizi Mkuuu wa Kituo cha Kitangiri Kati, eneo la Wazi namba Moja akiw-ongea na Wanahabari juu ya zoezi la uchaguzi katika kituo hicho ambapo amesema kuwa mambo yameenda shwari na hakukuwa na mapungufu makubwa mbali na baadhi ya wananchi kutotambua mapema majina yao yalipo katika Kata hiyo, japo changamoto hiyo imeshughulikiwa mapema.
Mwenye kofia ni Aloyce Mtani ambae ni Msimamizi wa Kituo cha Uchaguzi cha Bismack Jijini Mwanza akizungumza na Wanahabari
Kushoto ni Goodluck Masatu ambae niMtendaji wa Kata ya Kitangiri na msimamizi mkuu wa Uchaguzi katika Kata hiyo akiongea na Wanahari
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza nao wameelezea namna zoezi lilivyooenda na baada ya kupiga kura walikuwa wakirejea majumbani mwao
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza nao wameelezea namna zoezi lilivyooenda na baada ya kupiga kura walikuwa wakirejea majumbani mwao
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza nao wameelezea namna zoezi lilivyooenda na baada ya kupiga kura walikuwa wakirejea majumbani mwao
Piga Kura kwa Amani
Zoezi la Kupiga kira likiendelea mapema hii leo
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza nao wameelezea namna zoezi lilivyooenda na baada ya kupiga kura walikuwa wakirejea majumbani mwao
Wenye mahitaji maalumu nao wamepata usaidizi kwa uzuri kabisa
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza nao wameelezea namna zoezi lilivyooenda na baada ya kupiga kura walikuwa wakirejea majumbani mwao
BINAGI MEDIA GROUP, KWA PAMOJA TUIJUZE JAMII.
Kumbuka Uchaguzi Usitutenganishe, Zingatia Amani ndiyo Watanzania wanahitaji.

Mmoja wa wakazi wa Kijitonyama mpakani akipiga Kura yake
KITUO CHA KUPIGIA KURA NZASA
Baadhi ya wakazi wa Mtaa wa Nzasa wakiwa wanangoja kupiga Kura
Bado wakazi wa Nzasa wanangoja kupiga Kura
Baadhi ya wakazi wakihakiki majina yao ili kujua wanatakiwa wakae sehemu gani kabla ya kupiga kura
Ulinzi pia ukiwa umeimarishwa hali ni Shwari
Wengine wanaamua kungojea pembeni kidogo
Leo shughuli zimesimama kupisha uchaguzi mkuu
KITUO CHA KUPIGIA KURA CHA  KENTON
Baadhi ya wakazi wakihakiki majina yao kabla ya kuingia kwa ajili ya kupiga Kura 2015
Baadhi ya watu wakiwa wamepanga mistari kwa ajili ya kungoja kupiga kura
Kutokana na Foleni kuchangamka Baadhi yao wanaonekana kupumzika chini
Watu mbalimbali wakingojea kupiga Kura
watu wengi kituo cha Kenton
Waliokuwa wakichati wakachati sana kuperuzi na wengine wakawa bizee bizeee na kusoma Magazeti huku wakingojea Kupiga Kura 
KITUO CHA KUPIGIA KURA CHA USTAWI WA JAMII
Hapa ni Chuo cha Ustawi wa Jamii ambapo pia kuna watu wamejitokeza kwa wingi kupiga Kura
Bado wanaendelea kungojea
Wengine wamekaa wakisubili kupiga Kura
Baadhi yao wamesimama Pembeni wakingoja pia kupiga Kura
Mmoja ya wazee akiwa anasaidiwa kutembea kwenda kupiga Kura 
KITUO CHA KUPIGIA KURA CHA  MPAKANI A KIJITONYAMA
Wananchi wakiwa wamejitokeza kwa wingi kupiga kura katika kituo hiki cha Mpakani Kijitonyama
Kazi zikiwa zinaendelea
Umati wa watu ni Mkubwa lakini watu wanaendelea kungoja wapige Kura

Mmoja ya akinamama akiwa anapigia tiki viongozi ambao anawataka
 
Picha zote na Fredy Njeje-Blogs za Mikoa Tanzania