Matukio Katika Maadhimisho Siku ya Vijana Duniani…!

Baadhi ya vijana kutoka shule mbalimbali wakiandamana kuingia katika viwanja vya mnazi mmoja wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishwa  jijini Dar es Salaam. Mashirika mbalimbali  ya mataifa yanayofanya shughuli za vijana ni kamaUNFPA, IYF, UNIC, ILO, RESTLESS DEVELOPMENT, YUNA, AMREF, MARIE STOPES, pamoja na PSI.

Baadhi ya vijana kutoka shule mbalimbali wakiandamana kuingia katika viwanja vya mnazi
mmoja wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishwa jijini Dar es Salaam. Mashirika mbalimbali ya mataifa yanayofanya shughuli za vijana ni kamaUNFPA, IYF, UNIC, ILO, RESTLESS DEVELOPMENT, YUNA, AMREF, MARIE STOPES, pamoja na PSI.

 
 
Maandamano  yakiongozwa na bendi ya jeshi la polisi
 
 
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante
Ole Gabriel (wa tatu kutoka kushoto) pamoja na viongozi wengine wakipokea maandamano ya vijana wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishwa
katika Viwanja vya Mnazi Mmoja leo jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni
Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi na wapili kushoto ni
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu
duniani (UNFPA) Bibi. Natalia Kanem.
 
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante
Ole Gabriel pamoja viongozi wengine wakipokea maandamano ya vijana wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja  jijini Dar es Salaam.
 Viongozi katika meza kuu wakiimba wimbo wa Taifa wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja  jijini Dar es Salaam.
  Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa
linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem akizungumza
na vijana wakati wa Maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja. Katika hotuba yake aliweza kuzungumzia maswala ya watoto wa kike kubeba mimba wakiwa na umri mdogo ambao unapelekea kuacha masomo kutokana na ujauzito huo pia aliwasisitiza vijana kuwa na umoja kwani ndio nguvu kazi ya Taifa.
 
Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi(wa nne kutoka kulia) akimkaribisha mgeni rasmi kuzungumza na vijana wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.Wa tatu kutoka Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel, Wa kwanza kulia ni Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum na wa pili kutoka kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem.
 Naibu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole
Gabriel (kushoto) akitoa shukrani kwa wawakilishi wa Umoja wa Mataifa katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es
Salaam. Wa kwanza kulia ni Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  
wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum na wa pili kutoka kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem.
Naibu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akiwahutubia vijana walioshiriki maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake aliwasisitiza vijana kujitokeza katika uchaguzi unaotegemea kufanyoka mwezi wa kumi mwaka huu ili kuchagua viongozi makini watakaoweza kutetea masuala ya vijana na pia aliwasisitiza vijana kufanya kazi za kujitolea.
 Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja
wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum akiwasalimia vijana walioshiriki maadhimisho ya siku ya kimataifa ya
vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Bw. Hesein
Melele(wa kwanza kuli) kijana ambaye ni mwakilishi wa asasi ya vijana chini ya umoja wa mataifa
(YUNA) akiwasilisha maazimio yaliyofikiwa na vijana wakati wa kongamano
lililofanyika Agosti 10 mwaka huu kujadili ujumbe wa siku ya kimataifa ya
vijana duniani na kuandaa maazimio yaliyowasilishwa kwa mgeni rasmi leo katika
Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana
duniani.
 Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Jangwani, Tatu Ahmed akitoa shukrani kwa wageni waalikwa waliofika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani.
Mratibu wa Mkoa wa Dar es Salaam kutoka asasi ya vijana chini ya umoja wa mataifa (YUNA), Rahim Nasser akiwatolea ufafanuzi vijana waliofika kwenye banda la Umoja wa Mataifa katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani  Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akimsikiliza kwa makini Mratibu wa Mkoa wa Dar es Salaam kutoka asasi ya vijana chini ya umoja wa mataifa (YUNA), Rahim Nasser alipotembelea kwenye banda la Umoja wa Mataifa
 Mkufunzi wa Ujasiriamali/Biashara wa Program ya anzisha na imarisha biashara yako (SIYB) iliyochini ya Shirika la Kazi Duniani (ILO), Bw. MacDonald Lanzi (wa pili kutoka kulia) akimfafanulia jambo Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel. Wa pili kushoto ni Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum na wa kwanza kutoka kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem.
Mshauri na Mkufunzi wa Ujasiriamali/Biashara
wa Program ya anzisha na imarisha biashara yako (SIYB) iliyochini ya Shirika la
Kazi Duniani (ILO), Bw. Lawrence Ambokile(mwenye koti jeusi)
 akitoa ufafanuzi kwa Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel alipotembelea banda ilo
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akisaini kitabu katika kwenye moja ya bada la PSI Tanzania katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani. kushoto ni Dkt. Benedict Nyiro
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem akisaini kitabu katika kwenye moja ya bada la PSI Tanzania katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani. kushoto ni Dkt. Benedict Nyiro
 Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum akisaini kitabu katika kwenye moja ya bada la PSI Tanzania katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani. kushoto ni Dkt. Benedict Nyiro
Ofisa Habari wa Kituo cha Taarifa cha Umoja wa Mataifa Tanzania (UNIC), Stella Vuzo(wa kwanza kushoto), Meneja mradi wa ICS Bi. Imisa Masinjila(wa pili kutoka kushoto), Mkurugenzi wa Utamaduni kutoka Wizara hiyo Prof. Hermas
Mwansoko(wapili kutoka kulia) pamoja na 
Imisa Masinjila wakizungumza jambo maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum(wa kwanza kushoto) pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem(katikati) wakizungumza jambo na  Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi  wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya vijana waliofika kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 

  
 
 
 
 
 
 
 
 Vijana kutoka vikundi mbalimbali wakitoa burudani wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 
 
 
Vijana wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali yaliyokua yakiendelea wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Geofrey Adroph)