Matokeo ya Awali Uchaguzi wa Ubunge Arusha Mjini na Handeni Mjini

Baadhi ya Viongozi wa ChademaMatokeo ya Awali Uchaguzi wa Ubunge Arusha Mjini na Handeni Mjini
Taarifa za awali ambazo mtandao huu umezipata ni kwamba matokeo ya Ubunge Jimbo la Arusha Mjini; idadi ya wapiga kura walioandikishwa 317,814, Waliopiga kura 105,800 ikiwa sawa na 32.83%, Kura halali 104,353, Kura zilizoharibika 1447.

MATOKEO;

NAVOI MOLLEL ACT kura 342 sawa na 0.3%.

PHILEMON OLAIS MOLLEL CCM kura 35,907 sawa na 34.4%.

GODBLESS JONATHAN LEMA CDM kura 68,848 sawa na 65.9%.

ZUBERI MWINYI HAMIS CUF kura106 sawa na 0.1%.

MKAMA RASHID JARALIA kura 43 sawa na 0.04%.

Matokeo Jimbo la Handeni mjini; Waliojiandikisha kata zote 12 ni 38,597, waliopiga kura 16,046.

Matokeo; Kigoda Omar Abdullah wa CCM amepata kura 10,315 (75.90%)
Shundi Remmy Aidan wa CUF amepata kura 2,419 (17.80%),
Daudi Killo Lusewa wa CHADEMA amepata kura 648 (4.77%)
Hassan Mohamedi wa ADC amepata kura 184 (1.35%)
Na Bakari Makame Semndil wa TLP amepata kura 19 (0.14%).