Manchester City Yaibeba Uingereza Ligi ya Mabingwa Ulaya

city1

Michuano ya klabu bingwa barani Ulaya imeendelea tena usiku wa Jumatano kwa michezo miwili , Ambapo Klabu ya soka ya Manchester city imefanikiwa kuchomoza na ushindi mnono wa magoli 3-1 dhidi ya Dynamo Kiev .

city4

Magoli ya Manchester city katika mchezo huo yamefungwa na wachezaji Sergio Aguero dk15 , David Silva dk 40, huku bao la tatu likifungwa na Yahya Touré dk 90.Kwa upande wa Dynamo Kiev bao lao la kufutia machozi limefungwa na Vital Buyal-sky dk 58

city3

Katika mchezo mwingine Psv Eindhovein wakiwa nyumbani wametoshana nguvu na Atletico Madrid kufuatia sare tasa ya bila kufungana.

city2

Nayo PSV Eindhoven wakitoshana nguvu ya kutofungana dhidi ya Atletico Madrid, Michuano hiyo itaendelea tena March 8, 2016 kwa mechi mbili ambapo Real Madrid itaikaribisha Fc Roma na VfL Wolf- Sburg ikichuana na KAA Gent.