Madiwani Manispaa ya Lindi Wapata Mafunzo Juu ya Miradi ya UTT-PID

Mkurugenzi Mkuu wa UTT-PID, Dk. Gration Kamugisha (kulia) akielezea juu ya Taasisi hiyo juu ya utendaji wa kazi zake hapa Nchini, kushoto kwake ni Naibu Meya wa Manispaa ya Lindi, Amida Abdallah na pichani chini kulia ni Mstahiki Mstahiki Meya wa manispaa ya Lindi, Frank Magali.

Mkurugenzi Mkuu wa UTT-PID, Dk. Gration Kamugisha (kulia) akielezea juu ya Taasisi hiyo juu

ya utendaji wa kazi zake hapa Nchini, kushoto kwake ni Naibu Meya wa Manispaa ya Lindi, Amida Abdallah na pichani chini kulia ni Mstahiki Mstahiki Meya wa manispaa ya Lindi, Frank Magali.

Baadhi ya Madiwani wa Manispaa ya Lindi, wakiendelea na mafunzo hayo kutoka kwa maofisa wa UTT-PID (hawapo pichani)

Baadhi ya Madiwani wa Manispaa ya Lindi, wakiendelea na mafunzo hayo kutoka kwa maofisa wa UTT-PID (hawapo pichani).

Diwani akifuatilia mafunzo ya UTT-PID

Diwani akifuatilia mafunzo ya UTT-PID.

madiwani  wa Manispaa ya Lindi wakifuatilia mkutano huo wa UTT-PID jijini Dar es Salaamk

Madiwani wa Manispaa ya Lindi wakifuatilia mkutano huo wa UTT-PID jijini Dar es Salaam.

madiwani  wakifuatilia mkutano huo wa UTT-PID  uliokuwa unafanyika jijini Dar es Salaam

Pichani juu na chini ni madiwani wakifuatilia mkutano huo wa UTT-PID uliokuwa unafanyika jijini Dar es Salaam.

Mdiwani wakiendelea na mfunzo haayo ya UTT-PID

Madiwani wakiwa kwenye mafunzo hayo ya UTT-PID.

Madiwani wa Manispaa ya Lindi wapo jijini Dar es Salaam katika ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu iliyo chini Wizara ya Fedha (UTT-PID), iliyopo jijini Dar es Salaam na nje ya Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza na kuelewa utendaji wa kazi wa taasisi hiyo hapa nchini.

Katika ziara hiyo inayotarajia kumalizika Machi 19, mwaka huu. Mapema leo Machi 16, Madiwani hao wakiongozwa na Mstahiki Meya wa Manispaaa ya Lindi, Frank Magali waliweza kupatiwa elimu juu ya utendaji kazi wa taasisi hiyo ya UTT-PID na miradi inayoendesha hapa nchini.

Miongoni mwa elimu hiyo ni pamoja na ufanyaji wa kazi wa UTT-PID na wadau wanaoshirikiana nao huku hadi sasa ikiwa inasimamia miradi mbalimbali ikiwemo mikoa ya Pwani, Morogoro, Kagera, Dar es Salaam, Lindi na mikoa mingine hapa nchini.

Awali akiwakaribisha madiwani hao wa Manispaa ya Lindi, Mkurugezi Mkuu wa UTT-PID. Dk. Gration Kamugisha alieleza kuwa, UTT-PID imekua ikifanya kazi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo viongozi wa Siasa, wananchi, wadau na wabia binafsi pamoja na serikali katika kutekeleza mipango yake.

“Karibu sana UTT-PID, miradi yetu tunafanya kwa kushirikiana na watu mbalimbali. Wakiwemo wanasiasa, ndio maana leo tupo nanyi Madiwani ambao munawawakilisha wananchi huko munako toka” alieleza Dk. Gration Kamugisha.

Aiadha, kwa upande wa Madiwani hao walipongeza UTT-PID kwa hatua hiyo ya kuwapa elimu sambamba na kutembelea baadhi ya miradi inayoendeeshwa na taasisi hiyo.

Chanzo: Mo dewji blog