Kikwete Awataka Watanzania Kuboresha Kilimo Nanenane Lindi

Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akiwapungia mkono na kuwaaga wakulima na wafuagaji wakati wa kufunga Sherehe za Nane Nane mwishoni mwa wiki zilizofanyika Kitaifa katika uwanja wa Ngongo mkoani Lindi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akiwapungia mkono na kuwaaga wakulima na wafuagaji wakati wa kufunga Sherehe za Nane Nane mwishoni mwa wiki zilizofanyika Kitaifa katika uwanja wa Ngongo mkoani Lindi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akibonyeza kitufe kuashiria kuzinduliwa kwa Benki ya Maendeleo ya Kilomo nchini ambayo wakulima watapata huduma za kibenki ikowemo mikopo na kuwainua wakulima waweze kulima kwa uwezo wao. Hafla ya uzinduzi ilifanyika wakati wa kufunga Sherehe za Nane Nane Kitaifa mwaka huu zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Ngongo mkoani Lindi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akibonyeza kitufe kuashiria kuzinduliwa kwa Benki ya Maendeleo ya Kilomo nchini ambayo wakulima watapata huduma za kibenki ikowemo mikopo na kuwainua wakulima waweze kulima kwa uwezo wao. Hafla ya uzinduzi ilifanyika wakati wa kufunga Sherehe za Nane Nane Kitaifa mwaka huu zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Ngongo mkoani Lindi.

Baadhi ya wananchi wakisikiliza hotuba ya kufunga Sherehe za Nane Nane Kitaifa mwaka huu zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Ngongo mkoani Lindi kwa kuongozwa na kauli mbiu: “Matokeo Mkubwa Sasa, Tuchague Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo na Ufugaji”.

Baadhi ya wananchi wakisikiliza hotuba ya kufunga Sherehe za Nane Nane Kitaifa mwaka huu zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Ngongo mkoani Lindi kwa kuongozwa na kauli mbiu: “Matokeo Mkubwa Sasa, Tuchague Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo na Ufugaji”.

Baadhi ya wananchi wakisikiliza hotuba ya kufunga Sherehe za Nane Nane Kitaifa mwaka huu zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Ngongo mkoani Lindi kwa kuongozwa na kauli mbiu: “Matokeo Mkubwa Sasa, Tuchague Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo na Ufugaji”.

Baadhi ya wananchi wakisikiliza hotuba ya kufunga Sherehe za Nane Nane Kitaifa mwaka huu zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Ngongo mkoani Lindi kwa kuongozwa na kauli mbiu: “Matokeo Mkubwa Sasa, Tuchague Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo na Ufugaji”.

Baadhi ya wananchi wakitembelea baadhi ya bustani wakati wa kufunga Sherehe za Nane Nane Kitaifa zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Ngongo mkoani Lindi. (Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO, Lindi)

Baadhi ya wananchi wakitembelea baadhi ya bustani wakati wa kufunga Sherehe za Nane Nane Kitaifa zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Ngongo mkoani Lindi. (Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO, Lindi)


Na Eleuteri Mangi, Lindi

WATANZANIA wameaswa kuboresha sekta ya kilimo ili kuleta mapinduzi ya kijani katika sekta hiyo kwa kuzingatia na kutekeleza sera ya kilimo kwa manufaa ya wananchi wote na taifa kwa ujumla. Kauli hiyo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete mwishoni mwa wiki alipokuwa akiwaaga wakulima na wafugaji wakati wa kufunga Sherehe za Nane Nane Kitaifa zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Ngongo mkoani Lindi.

Rais Kikwete alisema kuwa amewaaga Watanzania ambapo anamini sekta ya kilimo, uvuvi na ufugaji wa wanyama pamoja na ufugaji wa nyuki nchini zimeongeza kutoa ajira na pato la taifa ambapo kilimo pekee kinachangia asilimia 25 hali inayowahakikishia wananchi kuwepo kwa chakula cha kutosha pamoja na malighafi.

Akihutubia wananchi waliohudhuria sherehe za kufunga maadhimisho hayo, Rais Kikwete alisema licha ya kuwa na mafanikio katika sekta ya kilimo na ufugaji zipo changamoto zinayoikabili sekta hiyo. Kwa mujibu wa Rais Kikwete, sekta kilimo inakabiliwa na changamoto kadhaa ambazo zinazuia sekta hiyo kuwa na uzalishaji bora wa mazao ambao utakuwa wenye tija kwa taifa na wananchi wake.

Changamoto hizo zinazorudisha nyuma kilimo ni pamoja na matumizi ya jembe la mkono, kutegemea mvua ya Mwenyezi Mungu ambayo nayo inakabiliwa na mabadiliko ya tabia nchi na matumizi ya mbegu za asili ambazo hazizai sana kulinganisha na mbegu za kisasa.

Changamoto nyingine ni matumizi madogo ya mbolea ambapo ardhi haina virutubisho vyote vinavyotakiwa ili kupata mazao ya kutosheleza mahitaji kulingana na idadi ya watu na kuwa na chakula cha ziada. Ujuzi mdogo wa wakulima katika kupanda mbegu mashambani nao umekuwa kikwazo katika mapinduzi ya kilimo ambapo Rais alitoa mfano ambao unaonesha kuwa zao la mhogo likipandwa kitaalam heka moja inapaswa kuwa na miche 2500 ili kutoa mazao bora na yenye tija ukilinganisha na hali ilivyo sasa nchini.

“Changamoto nilizoziainisha zinazoikabili sekta ya kilimo, sasa zimepatiwa ufumbuzi wa kudumu kwa wakulima wetu ambapo tutazindua Benki ya Maendeleo ya Kilomo nchini ambayo wakulima watapata huduma za kibenki, mikopo na kuwainua wakulima kulima kwa uwezo wao na kuimarisha vituo vya utafiti wa kilimo na mifugo nchini.

Sasa Tanzania na Afrika imeanza safari ya kulipeleka jembe la mkono kwenye jumba la makumbusho” alisema Rais Kikwete.
Akionesha mafanikio katika kilimo katika uongozi wake Rais Kikwete alisema kuwa utegemezi wa jembe la mkono umepungua kutoka asilimia 62 hadi 70, matumizi ya wanyama kazi kwa ajili ya kilimo yameongezeka kutoka asilimia 20 hadi 24 na matrekta nchini yameongezeka kutoka asilimia 10 hadi asilimia 14 ambapo kwa sasa kuna mtrekta 16412.

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Stephen Wassira akimkaribisha Rais kuhutubia na kufunga Maonesho ya Nane Nane Kitaifa alitoa wito kwa kanda zote nchini kuendeleza mabanda yaliyopo katika viwanja wa maonesho ya wakulima nchi nzima ili viwe shamba darasa na kwa kuwa na tija kwa wakulima na wafugaji.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Kilimo Taifa (TASO) Englebert Moyo amewapongeza washiriki wote kwa kuonesha teknolojia sahihi wakati wote wa maonesho inayowalenga wakulima na wafugaji na ambayo wanaweza kuitumia katika mazingira yao.
Maonesho ya Nane Nane nchini yameanzishwa rasmi mnano mwaka 1993 ambapo hadi sasa yanaendelea nchini kupitia kanda ya Arusha, Dodoma, Morogoro, Mbeya na Mwanza na Lindi ambapo maonesho hayo yanafanyika kitaifa kwa mara ya pili mfululizo na yanatarajiwa kuhitimishwa 2018 kwa kanda ya kusini baada ya kuongezewa miaka miwili ya kuwa wenyeji na waandaji wa maonesho hayo kitaifa. Kauli mbiu ya Manesho ya Nane Nane mwaka huu ni “Matokeo Mkubwa Sasa, Tuchague Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo na Ufugaji”.

Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Mwajuma Msina akitoa maelezo kwa wageni waliotembelea banda la wizara hiyo wakati wa Maonesho ya Nane Nane kitaifa yanayoendelea katika uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.

Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Mwajuma Msina akitoa maelezo kwa wageni waliotembelea banda la wizara hiyo wakati wa Maonesho ya Nane Nane kitaifa yanayoendelea katika uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.

Mtafiti wa kilimo kutoka taasisi ya Utafiti Kilimo Naliendele Festo Masisila akiwaeleza wakulima Thomas Mihambo (katikati) na Zuhura Nalipa (kulia) kutoka mtaa wa Mbawala Chini kata ya Naliendele mkoani Mtwara namna bora ya kulima zao la mhogo ikiwemo aina ya Kiroba, Pwani, Kizimbani, Makutupora, Dodoma, Mkumba na Mkuranga 1 inayostawi vizuri mkoani Mtwara wakati wa Maonesho ya Nane Nane kitaifa yanayoendelea katika uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.

Mtafiti wa kilimo kutoka taasisi ya Utafiti Kilimo Naliendele Festo Masisila akiwaeleza wakulima Thomas Mihambo (katikati) na Zuhura Nalipa (kulia) kutoka mtaa wa Mbawala Chini kata ya Naliendele mkoani Mtwara namna bora ya kulima zao la mhogo ikiwemo aina ya Kiroba, Pwani, Kizimbani, Makutupora, Dodoma, Mkumba na Mkuranga 1 inayostawi vizuri mkoani Mtwara wakati wa Maonesho ya Nane Nane kitaifa yanayoendelea katika uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.

Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Mwajuma Msina akiongea na wanafunzi wa shule ya Msingi Kitangali Mazoezi kutoka wilaya ya Newala Mkoani Mtwara kujua namna watoto wanavyonufaika na mfuko huo wakati wa Maonesho ya Nane Nane kitaifa yanayoendelea katika uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.

Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Mwajuma Msina akiongea na wanafunzi wa shule ya Msingi Kitangali Mazoezi kutoka wilaya ya Newala Mkoani Mtwara kujua namna watoto wanavyonufaika na mfuko huo wakati wa Maonesho ya Nane Nane kitaifa yanayoendelea katika uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.


Afisa Masoko UTT-PID, Bi Kilave Atenaka akihudumia mteja katika banda lao lililo chini ya wizara ya Fedha katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.

Afisa Masoko UTT-PID, Bi Kilave Atenaka akihudumia mteja katika banda lao lililo chini ya wizara ya Fedha katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.

Maafisa Masoko wa UTT-PID, Bi Kilave Atenaka (katikati) na  Bi. Mary Minja (kwanza kulia) wakiongea na mteja aliyefika banda lao lililo chini ya wizara ya Fedha katika Maonyesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.
Afisa Masoko UTT-PID, Bi Kilave Atenaka akihudumia mteja katika banda lao lililo chini ya wizara ya Fedha katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.
 
 Muonekano wa viwanja vya Mabano vilivyopimwa na Taasisi ya UTT-PID kwa ushirikiano na Halmashauri vilivyopo Manispaa ya Lindi.

Zaidi ya viwanja 2,500 vilipimwa kwa ajili ya matumizi mbalimbali kama vile Makazi, Biashara, Maeneo ya Umma na sehemu za kupumzika.  
 Akielezea Afisa Masoko Bi. Kilave Atenaka alisema kuwa kwa sasa wanaendesha huduma ya uuzwaji wa Fomu kwa ajili ya Viwanja, pia wanatarajia kuanza kuuza kwa umaa na taasisi mbali mbali miradi mipya ikiwemo wa Tundwi Songai – Kigamboni jijini Dar es Salaam na ule wa Kingorwila, Morogoro.

Aidha Bi. Kilave alitumia wito huo kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi ndani ya banda hilo kujipatia elimu mbali mbali zitolewazo na taasisi hiyo hapa nchini.

Toka kuanzishwa kwake Taasisi ya UTT-PID imejikita sana katika upimaji wa maeneno katika mikoa mbalimbali kwa kushirikiana na Halmashauri tofauti nchini. Miradi mikubwa kama ya Bukoba ambapo viwanja zaidi ya 5,000 vilipima kuuzwa, Halmashauri ya Sengerema kwa ushirikiano na Taasisi ilipima zaidi ya viwanja 1,200 na uuzaji pamoja na uwekezaji katika Miundombinu husika unaendelea kwa kasi. Pia Taasisi imewekeza katika miradi binafsi kama vile eneo la Mapinga katika wilaya ya Bagamoyo huku ikatarajia uwekezaji mkubwa zaidi katika mikoa ya Morogoro , Arusha, Dar es Salaam, Maswa, Pwani, Maswa na Ruvuma.