Ijue Teknolojia Mpya Katika Sekta ya Rangi

Ijue Teknolojia Mpya Katika Sekta ya Rangi
Ijue Teknolojia Mpya Katika Sekta ya Rangi
Ijue Teknolojia Mpya Katika Sekta ya Rangi
KUFUATILIA kukua kwa teknolojia ya kompyuta kwa sasa sekta tofauti tofauti zimeweza kuchukua fursa hiyo na kuitumia ipasavyo katika maeneo ya msingi; sekta ya upakaji rangi pengine ni moja kati ya ambazo mtu hawezi kuzihusisha moja kwa moja na maendeleo hayo ila hata hivyo imeweza kuendana na mabadiliko na kuitumia teknolojia katika hatua tofauti tofauti kuanzia viwandani mpaka maeneo ya masoko. Manufaa ya teknolojia hayawafaidishi tu wazalishaji ila pia wadau wa biashara, mawakala na mwisho kabisa mtumiaji.

Matumizi ya teknolojia ya kompyuta katika maeneo ya kuuzia yamefanya mapinduzi katika namna ambazo watu wananunua vitu, shughuli iliyokuwa inafanyika muda mrefu kwa kutumia wafanyakazi sasa zinamalizika ndani ya dakika chache. Miongoni mwa mabadiliko ya kiteknolojia ambayo yamekuwa muhimu katika kujenga hali hii ni mfumo wa uchanganyaji rangi unaotumika na wadau ujulikanao kimataifa kama DTS.

Mfumo otomatiki wa kuchanganya rangi unatumia mchanganyiko wa vichupa vya rangi, kichanganyio na kompyuta mpakato maarufu kama ‘Laptop’ ambavyo vinaunda mfumo huu wa DTS. Ikiwa moja kati ya juhudi za kundeleza sekta ya rangi, kampuni inayoongoza kwenye uzalishaji wa rangi nchini Insignia (Coral Paints) wamekuwa vinara katika kuitambulisha teknolojia hii nchini. Miaka 8 iliyopita kampuni hii ilikuwa ya kwanza kuleta wazo la kuitumia sokoni na kwa miaka mingi imekuwa na mikakati ya kuhakikisha kuwa manufaa yanawafikia wote kwa kuwawekea technolojia hii wadau wake na wasambazaji nchini.

Vifaa hivyo vinawekwa katika maeneo ya wasambazaji na zina ruhusu mabadiliko yoyote ya uzalishaji wa rangi kulingana na anavyotaka mteja. Kwa wasambazaji mbinu hii inaleta faida mbalimbali kiuchumi ikiwa ni pamoja na kupunguza mzigo kwani msambazaji hatahitaji kuwa na mzigo mkubwa. Badala ya kuhifadhi rangi nyingi tofauti tofauti, msambazaji anahitaji kuhifadhi rangi kuu na tona na kwa kutumia mashine hiyo ana kua na uwezo wa kutengeneza rangi yoyote katika kadi hapo hapo. Mashine hii inachanganya kwa kutumia rangi za msingi. Ni mali muhimu ki biashara kwa muuzaji ambayo inarahishisha uendeshaji na kumawasaidia kuepuka kuishiwa na akiba au kukaa na bidhaa zisizo na muhimu.

Tangu kutambulishwa kwake DTS imekuwa chaguo la msingi kwa wadau wengi katika sekta ya rangi. Bw. Kishan Dhebar, Mkurugenzi Mtendaji wa Coral Paints, anaelezea kwamba “DTS ina faida kadhaa na imekuwa mshirika wa karibu katika kukuza maendeleo ya sekta ya rangi. Mzigo mdogo na matokeo ya haraka inasaidia kuridhisha wateja ambapo pia inaongeza mafanikio kwa mfanya biashara” Bw. Kishan pia akiongelea manufaa ambayo mtumiaji wa mwisho anapata kwa kutumia teknolojia hii wakati wa kununua anasema “gharama ya kuchanganya rangi katika mashine ni ndogo kuliko kununua rangi hiyo ikiwa imesha changanywa kutoka kiwandani kutokana na bei ndogo ya rangi za msingi. Bidhaa nyingi zinaweza kutumika katika mashine kuzalisha rangi mbalimbali. Hivyo wateja hawafaidiki tu kwa gharama kuwa nafuu lakini pia wanaokoa muda sababu ya huduma ya papo kwa hapo na uhakika wa upatikanaji wa zaidi ya michanganyiko 10,000”

Wakiwa wamekamata sehemu kubwa ya soko la rangi na sekta ya upakaji rangi na wakiendelea kusukuma nia ya ugunduzi katika nyanja tofauti tofauti Coral Paints wanaendelea kushikilia nafasi yao ya uongozi kwenye sekta ya rangi Tanzania siyo tu kwa wingi/ujazo na thamani lakini pia kupitia kutambulisha na kutumia teknolojia mpya pamoja na kuongoza hatua ambazo zimekuwa zikifungua njia.