Greg Dyke Awapiga Mkwara UEFA

England

Mwenyekiti wa chama cha mpira cha Uingereza, Greg Dyke amewaandikia barua chama cha shirikisho la soka barani Ulaya,UEFA kutoa maelezo ya tija kuhusu mpangilio wa ulinzi wakati wa michuano ya soka ya Euro 2016.

Leo Urusi itacheza katika mji wa Lile ambapo mashabiki wa Uingereza pia watakusanyika hapo kwa kuwa mechi yao itakuwa kesho.

Kulikuwa na usumbufu mkubwa katikati hapo wakati timu zote zilipopangwa mwishoni mwa juma.Mashabiki sita wa England wamefungwa kutokana na vurugu zilizotokea lakini hakuna yeyote kati ya mamia ya mashabiki wa Urusi aliyewekwa hatiani,Maafisa wa Ufaransa wameliita tukio hilo kuwa ni vurugu za kihuni,hivyo timu zote mbili zilipaswa kutolewa katika michuano kama patatokea vurugu nyingine.