FIFA Yaipa Onyo Kali Shirikisho la Soka Nchini Nigeria

fifa

Shirikisho la kandanda duniani limetishia kuipiga marufuku Nigeria kutoka kwenye mashindano yeyote ya kimataifa iwapo haitamrejesha afisini rais wa NFF Amaju Pinnick mara moja.

Rais wa NFF Amaju Pinnick aliondolewa madarakani Alhamisi iliyopita baada ya mahakama moja ya Jos kuamua kuwa kiongozi wa sasa Pinnick alishindwa katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka wa 2014.

Mahakama ilisema kuwa Chris Giwa ndiye anayefaa kuwa rais wa shirikisho la soka la Nigeria NFF.

FIFA imeonya kuwa Nigeria imo katika hatari ya kupigwa marufuku endapo itatekeleza uamuzi wa mahakama.

Katika taarifa iliyotumwa kwa serikali ya Nigeria Jumatatu tarehe 11 Aprili kaimu katibu wa FIFA Markus Kattner, anasema uamuzi huo wa mahakama unatafsiriwa kama kuingiliwa kati kwa maswala ya kandana.