Dada Antu Mandoza Auomba Ubunge Viti Maalum Bukoba…!

Binti Antu Mandoza akirudisha fomu za kuwania nafasi ya Ubunge Vijana Viti Maalumu kupitia CCM. Akihojiwa alisema amedhamiria kuinua maisha ya vijana kwa kuwatengenezea fursa na mbinu mbalimbali za kujiajiri, pia kutokukubali kutumika vibaya na makundi ya Kisiasa tunapoelekea Uchaguzi Mkuu kwani ni wajibu wetu ijana kuilinda amani yetu. Mgombea huyo pia ameeleza shauku yake kubwa ni kuwatumikia Vijana kwa kutatua changamoto ya Ajira na pia ametoa ahadi ya kushirikiana na Vijana bega kwa bega kuleta maendeleo katika Mkoa wa Kagera.

Binti Antu Mandoza akirudisha fomu za kuwania nafasi ya Ubunge Vijana Viti Maalumu kupitia CCM. Akihojiwa alisema amedhamiria kuinua maisha ya vijana kwa kuwatengenezea fursa na mbinu mbalimbali za kujiajiri, pia kutokukubali kutumika vibaya na makundi ya Kisiasa tunapoelekea Uchaguzi Mkuu kwani ni wajibu wetu ijana kuilinda amani yetu. Mgombea huyo pia ameeleza shauku yake kubwa ni kuwatumikia Vijana kwa kutatua changamoto ya Ajira na pia ametoa ahadi ya kushirikiana na Vijana bega kwa bega kuleta maendeleo katika Mkoa wa Kagera.

Mgombea Ubunge Viti Maalum Vijana Bukoba Bi. Antu Mandoza(Kulia) akirejesha Fomu ya Kuomba Ridhaa kuteuliwa kugombea Ubunge wa Viti maalum Vijana Bukoba katika ofisi za umoja huo Mjini Bukoba, ahaidi kuinua Vijana Kiuchumi endapo atapata nafasi ya kuwa Mbunge wa Vijana.
Binti Antu Mandoza akiweka sawa Kumbukumbu zake katika kitabu mbele ya karani Bi. Jasinta Benedicto wa Umoja wa Vijana Kagera.
Dada Antu Mandoza akiwa kwenye Ofisi za Umoja wa Vijana BukobaMgombea Ubunge Viti Maalum Vijana Bukoba Dada Antu Mandoza (kulia) akiptia Fomu yake ya Kuomba Ridhaa kuteuliwa kugombea Ubunge wa Viti maalum Vijana. Kushoto ni Bi. Jasinta Benedicto karani wa Umoja wa Vijana Kagera.
Mgombea Ubunge viti maalumu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Antu Mandoza akitoka katika ofisi za umoja wa vijana wa CCM Mkoa wa Kagera baada ya kuchukua fomu. (Habari Picha na Faustine Ruta/bukobasports)