Mke wa Rais Magufuli, Mama Janeth Asaidia Vyakula Vituo vya Yatima

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimkabidhi Hajat Mwanaisha Magambo mkuu wa kituo cha New Life Orphanage cha Boko Dawasco kwa niaba ya viongozi wa vituo nane vya kulelea yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu waliopewa vyakula kwa ajili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani pamoja na sikukuu ya Eid el Fitr na Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam leo Juni 20, 2017. Vituo vilivyopkea vyakula hivyo ni pamoja na New Life kilichopo Boko Dawasco chanye watoto 121, Charambe Islamic kilichopo Charambe (watoto 54), Mwandaliwa Centre kilichopo Mbweni (watoto 94) Al Madina Children Home cha Tandale ( watoto 65), Ijangozaidia Orphanage Centre kilichopo Sinza (watoto 1030, Azam Orphanage kilichopo Mbagala (watoto 51), Hiari Orphanage kilichopo Chang’ombe (watoto41) na CHAKUWAMA (watoto 64) kilichipo Sinza.

 

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na viongozi wa vituo nane vya kulelea yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu kabla ya kuwakabidhi vyakula kwa ajili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani pamoja na sikukuu ya Eid el Fitr Ikulu jijini Dar es salaam leo Juni 20, 2017.

 

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na viongozi wa vituo nane vya kulelea yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu kabla ya kuwakabidhi vyakula kwa ajili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani pamoja na sikukuu ya Eid el Fitr Ikulu jijini Dar es salaam leo Juni 20, 2017.