Ukisikia Kuvuja Kwa Pakacha Ndio Huku

flamin

Crystal Palace wamemchukua kiungo wa kati wa zamani wa Arsenal Mathieu Flamini, ambaye alikuwa amesalia kuwa ajenti huru baada ya kuruhusiwa kuondoka na klabu ya Arsenal majira ya joto.

Flamini, 32, amepewa mkataba wa hadi mwisho wa msimu. Mchezaji huyo aliondoka kwa Gunners baada ya kucheza mechi 246 vipindi viwili na kushinda vikombe vya FA mara tatu.

Mfaransa huyo pia alishinda Serie A mwaka 2011 miaka mitano aliyokaa AC Milan. Ndiye mchezaji wa tano kununuliwa na Palace kwa mkataba wa kudumu majira ya sasa.

Flamini alihamia Italia baada ya kukaa miaka minne Arsenal kisha akarejea Emirates mwaka 2013. Palace wamewanunua pia Andros Townsend, Steve Mandanda, James Tomkins, na Christian Benteke. Wamempokea pia Loic Remy kwa mkopo kutoka Chelsea.