Leicester, Tottenham Waongoza Kutoa Wachezaji Bora

leicester-city-tottenham_hv66jzp9m08q14li8yp7s1nht

Timu za Leicester City na Tottenham imetoa wachezaji nane katika kikosi cha mwaka cha wachezaji bora wa wakulipiwa (PFA) wa ligi kuu ya England.

kila timu ikiwa imetoa wachezaji wanne wa kikosi hicho bora cha msimu huu,Washambuliaji Jamie Vardy na Harry Kane kuu ndio wanaongoza safu ya mashambulizi ya kikosi hicho

Kiungo wa Kijeruman Mesut Ozil ambae anawania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa chama cha wanasoka wa kulipwa PFA hayumo kwenye kikosi hicho.

PFA walikua wakitangaze kikosi hicho siku ya jumapili ijayo katika sherehe za utoaji tuzo lakini kwa sababu ya siri za kikosi kuvuja ikawabidi chama hicho kutangaza mapema kabla ya siku waliyopanga.