Simba Yaendelea Kung’ang’ania Kileleni Ligi Kuu

simba

Klabu ya Simba bado imeendelea kutamba kwenye ligi ya Vodacom Tanzania bara baada ya kuinyamazisha Tanzania Prisons ya Mbeya kwa bao 1-0 kwenye mchezo wa raundi ya pili ya ligi uliochezwa kwenye uwanja wa taifa jana.

Bao pekee lililoipa pointi tatu Simba limewekwa kambani dakika ya 86 na kiungo Awadh Juma kwa shuti kali akiwa nje ya box la 18 na kupeleka shangwe mtaa wa Msimbazi, Kariakoo

Michezo mingine iliyochezwa March 13 kwenye viwanja vingine matokeo yake ni
Majimaji 1-0 Stand United
Kagera Sugar 3-0 Coastal Union
Mgambo JKT 1-1 Mwadui FC