Mfumuko Bei za Vyakula Walitesa Soko Kuu Mwanza

Mmoja wa wafanyabiashara katika Soko Kuu Jijini Mwanza akieleza hali ya mfumuko wa bei ilivyo sokoni hapo

Mmoja wa wafanyabiashara katika Soko Kuu Jijini Mwanza akieleza hali ya mfumuko wa bei ilivyo sokoni hapo

Kwa takribani Wiki mbili sasa, Mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali kupanda katika Soko Kuu la Jijini Mwanza umeendelea kuwaliza watumiaji wa soko hilo.
Mfumuko huo unalalamikiwa na pande zote mbili kwa maana ya wauzaji na wanunuaji sokoni hapo, ambapo wameomba hatua za haraka kuchukuliwa ili kiweka mambo sawa.
Bei kwa nafaka zote sokoni hapo zimepanda bei hadi shilingi 1,000 kwa kila moja tofauti na hapo awali ambapo bidhaa iliyokuwa ikiuzwa shilingi 15,000 sasa inauzwa kati ya 2,000 hadi 2,500 ambapo steki ya nyama imepanda bei kutoka shilingi 5,000 hadi shilingi 8,000 huku nyama mchanganyiko ikiuzwa shilingi 6,000 kutoka 4,000 za awali.
Mwenyekiti wa Soko hilo Hamad Nchola amesema kuwa mfumuko huo umesababisha na mazao ya wakulima kupungua katika maghala yao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uhaba wa mavuno kutokana na ukosefu wa mvua katika msimu uliopita, pamoja na wafanyabiashara kutoingiza sokoni bidhaa katika kipindi cha uchaguzi mkuu, ambapo amewasihi wafanyabiashara kurejea katika mzunguko wao wa biashara kama kawaida hatua ambao itasaidia kukabiliana na mfumko huo wa bei.
Mmoja wa wauzaji wa nyama katika Soko Kuu Jijini Mwanza akieleza hali ya mfumuko wa bei ilivyo sokoni hapo
Mmoja wa wauzaji wa nyama katika Soko Kuu Jijini Mwanza akieleza hali ya mfumuko wa bei ilivyo sokoni hapo
Bei ya Nyama imepanda bei maradufu
Mteja akiteta na mwanahabari juu ya mfumuko wa bei katika Soko Kuu la Jijini Mwanza
Shughuli za kibiashara katika Soko Kuu Jijini Mwanza zikiendelea
Mmoja wa akina mama wanaouza chakula Soko Kuu Jijini Mwanza anasema kuwa mfumuko huo wa bei umesababisha biashara zao kukamwa
Kushoto ni Mwenyekiti wa Soko Kuu Jijini Mwanza Hamad Ntola akizungumza na Mwanahabari ofisini kwake juu ya mfumuko wa bei katika Soko hilo
Imeandaliwa na Binagi Media Group,Mwanza.