Mgombea Urais CCM, Dk Magufuli Akanyaga Kilomita 13,720

wananchi waliofurika kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za Urais,uliofanyika katika uwanja wa Kawawa, mkoani Kigoma wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dk. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia.

wananchi waliofurika kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za Urais,uliofanyika katika uwanja wa Kawawa, mkoani Kigoma wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dk. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,kupitia chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwahutubia  maelfu ya wananchi waliofurika kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za Urais,uliofanyika katika uwanja
wa Kawawa,mkoani Kigoma. 
 Dk. Mafuli amewaabia wananchi wa Kigoma kwenye mkutano wa kampeni leo jioni kwenye uwanja wa kawawa kuwa Serikali yake kwa sehemu kubwa itakuwa upande wa wananchi wanyonge ili hatimaye wawe na maisha yenye neema,amesema kuwa Serikali yake haitakuwa ya kunyanyasa mama ntile na kudaiwa kodi za hovyo hovyo, amesema kuwa ataimarisha ukusanyaji wa kodi kwenye serikali yake, lakini pia atawabana wafayabiashara  wakubwa ambapo baadhi yao
hawalipi kodi’
 
Magufuli amewataka Wananchi kumuamini kwa yale ambayo amekuwa akiyasema kwenye mikutano yake ya kampeni na
kuongeza anachoahidi ndicho ambacho atakitekeleza kwenye serikali yake na kwenye maisha yake huwa hataki kutoa ahadi za uongo.
 
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,kupitia chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwahutubia  maelfu ya wananchi waliofurika kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za Urais,uliofanyika katika uwanja wa Kawawa, mkoani Kigoma.

Aidha hadi jana, tarehe 16 September 2015, Mgombea Urais wa CCM, Dk. John Pombe Magufuli, alikuwa amekwishafanya kampeni katika mikoa 12 na Majimbo 94. Amekwishafanya mikutano mikubwa ya hadhara 76 na mikutano ya barabarani 381. Amekwishatembea, kwa gari, jumla ya kilomita 13,720. Kwa ujumla amekwishakutana, moja kwa moja, na asilimia zaidi ya 30 ya wapiga kura.

Wananchi na Mabango yao
Mgombea Urais wa CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Nguruka kwenye mkutano wa kampeni wa hadhara mapema.
Wakazi wa Nguruka wakifuatilia Mkutano.
Mgombea Urais wa CCM Dk. Magufuli akimkabidhi Ilani ya chama cha CCM kwa Mgombea Ubunge wa Kigoma Kusini, Hasna Mwilima na pia kummwombea kura kwa wananchi kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika
Nguruka mkoani Kigoma.
Wananchi wakisikiliza sera za Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli
Baadhi ya Wananchi wa Uvinza wakiwa wamefunga barabara wakitaka wasikilizwe kero zao na Mgombea Urais wa CCM, Dk. Magufuli alipokuwa akipita mjni humo akielekea Kigoma mjini kwenye mkutano wa hadhara.
Baadhi ya akina mama wakishangilia jambo
Mgombea Ubunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini Peter Selukamba akiwahutubia wananchi wa Kalinzi,mkoani Kigoma kweny mkutano wa kampeni za Uraisi.
Baadhi ya wafuasi wa chama cha CCM wakifuatilia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kalinzi, ambapo mgombea Urais wa CCM Dk. Magufulia aliwahutubia wananchi.
Wakazi wa mji wa Nguruka,mkoani Kigoma wakifuatilia mkutano wa hadhara
Wananchi na mabango yao
Kada maarufu na aliyewahi kuwa Katibu MKuu wa CCM, Yusuph Makamba akisalimiana na Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia chama cha CCM Dk. John Pombe Magufuli kabla ya kupanda jukwaani na kuwaomba ridhaa wakazi wa kigoma ya kuwaongoza katika awamu ya tano.
Wananchi wakishangilia jambo kweye mkutano wa kampeni za Urais
 
Wananchi wakifuatilia mkutano wa kampeni

Kada maarufu na aliyewahi kuwa Katibu MKuu wa CCM, Yusuph Makamba akiwahutubia wananchi wa Kigoma na vitongoji vyake kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za Urais, uliofanyka katika uwanja wa Kawawa mkoani Kigoma. 

PICHA NA MICHUZI JR-KIGOMA.