Cecafa Kagame Cup Kutimua Vumbi Jumamosi Dar

Cecafa Kagame Cup

Cecafa Kagame Cup


MICHUANO ya Kombe la Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa Kagame Cup) inatarajiwa kuanza kutimua vumbi siku ya Jumamosi tarehe 18 Julai 2015 jijini Dar es salaam, kwa kushirikisha timu 13 kutoka nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Soka kwa Nchi za Afrika Mashariki na kati.

Mashindano ya CECAFA Kagame Cup ni mashindano makongwe barani Afrika ambayo yalianza mwaka 1967 kwa kushirikisha timu za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, na mwaka huu ni mashindano ya 40 tangu kuanza kwa michuano hiyo. Klabu ya Simba ndio timu inayoongoza kwa kutwaa ubingwa huo mara sita (6) ikifuatiwa na Yanga, Gor Mahia zilizotwa mara (5), APR ya Rwanda ikiwa imetwaa ubingwa huo mara tatu (3). Yanga na Gor Mahia zina nafasi ya kufikia Simba SC endapo zitafanikiwa kutwaa Ubingwa msimu huu.

Mechi ya ufunguzi siku ya jumamosi uwanja wa Taifa itawakutanisha APR ya Rwanda dhidi ya Al Shandy ya Sudan saa 8 kamili mchana, KMKM kutoka Visiwani Zanzibar watacheza dhidi ya Telecom ya Djibout uwanja wa Karume saa 10 jioni, huku wenyeji timu ya Yanga wakiwakaribisha Gor Mahia kutoka Kenya saa 10 jioni.

Kuelekea kwenye mashindano hayo, waandaji wa michuano hiyo CECAFA kwa kushirikiana na wenyeji Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limetangaza viingilio vya michezo hiyo, ambapo Uwanja wa Karume kiingilio kitakua shilingi elfu mbili (2,000) na uwanja wa Taifa kiingilio cha chini kitakua ni shilingi elfu tano (5,000) na kiingilio cha juu ni elfu 20,000 (20,000).

Timu zinazoshiriki michuano hiyo
Kundi A: Yanga (Tanzania Bara), Gor Mahia (Kenya), Telecom (Djibout), KMKM (Zanzibar), Khartoum-N (Sudan).
Kundi B: APR (Rwanda), Al-Shandy (Sudan),LLB AFC (Burundi), Heegan FC (Somalia).
Kundi C: Azam FC (Tanzania), Malakia (Sudan Kusini), Adama City (Ethiopia) na KCCA (Uganda). Michuano hiyo ya CECAFA Kagame Cup itaonyeshwa moja kwa moja na kituo cha luninga cha Supersport.

UCHAGUZI TWFA
Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Soka cha Wanawake chini (TWFA) inatangaza kuwa wafuatao wamepita katika mchujo wa awali katika nafasi walizoomba kama ifuatavyo:
1. Amina Ali Karuma – Mwenyekiti
2. Devotha John Marwa – Mwenyekiti
3. Cecilia Makafu – Katibu Msaidizi
4. Somoe Roberst Ng’itu – Katibu Msaidizi
5. Debora Ernest Mkemwa – Mjumbe Kamati ya Utendaji
6. Mwanaheri Kalolo – Mjumbe Kamati ya Utendaji
7. Theresia Reginald – Mjumbe Kaamti ya Utendaji

Hivyo mtu yeyote mwenye pingamizi anaombwa aliwasilishe katika ofisi za TFF – Karume kuanzia tarehe 15/07/2015 mpaka 20/07/2015.