Ajali ya kutisha, 15 wafa, 67 wajeruhiwa

 

Na Mwandishi Wetu
Geita

WATU 15 wakiwemo watoto wawili, askari polisi mmoja wa

jijini Mwanza wamepoteza maisha na wengine 67 kujeruhiwa

vibaya katika ajali iliyohusisha basi la kampuni ya

Sheraton lenye namba T 268 AJC na basi la Bunda Expres

namba T 810 BDW baada ya kugongana uso kwa uso eneo la

Kijiji cha Chibingo Wilaya ya Geita mkoani Mwanza.

Ajari hiyo ambayo imetokea jana mjini hapa majira ya saa

tatu asubuhi eneo la barabara kuu ya Mwanza-Bukoba

imehusisha mabasi mawili pamoja na roli la mizigo aina

ya Fusso lenye namba za usajili T 823 BDV baada ya basi

la Sheraton lililokuwa likitoka Ushirombo Shinyanga

kwenda Mwanza, kutaka kulipita lori lililokuwa likipanda

kilima cha Chibingo.

Taarifa zinaeleza kuwa kabla ya kulipita gari hilo

lilikutana uso kwa uso na basi la Bunda lililokuwa

likitoka mkoani Mwanza kuelekea Karagwe Mkoa wa Kagera

na ndipo ajali hiyo ilipotokea.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wamesema ajali hiyo

imesababishwa na mwendo kasi wa madereva wa mabasi hayo

huku yule wa basi la Sheraton akitupiwa lawama kwa

kushindwa kufuata sheria za barabarani kutokana na

kutaka kulipita gali lililokuwa kwenye kilima bila

kuhofia atari yoyote eneo hilo.

“Tulikuwa tukitokea Shinyanga kwenda Mwanza na basi la

Sheraton tulipofika Kijiji cha Chibingo dereva wetu

alijalibu kulipita gari la mizigo, lakini alishindwa

kulimudu gari kisha kugongana uso kwa uso na basi la

Bunda hali iliyosababisha vifo…huu ni ukiukaji wa

sheria za barabarani,” alisema, Yunusu Mathias.

Mmmoja wa majeruhi, Johnas Kalokola ambaye ni mwanafunzi

wa Sekondari ya Ihungo Bukoba, alisema dereva wa Bunda

alijitahidi kulikwepa basi la Sheraton kwa kunusuru

maisha ya abiria waliokuwa wakisafiri kuelekea Karagwe,

lakini kutokana na mwendo kasi wa mabasi hayo

yaligongana na baadhi ya abilia kupoteza maisha, viungo

vya mwili na mali zao.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Geita, Dk.

Abdallah Dihenga amethibitisha kupokea miili 15 na

majeruhi zaidi ya 60 na kuongeza kati yao watu sita

wamepelekwa katika hospital ya rufaa ya Bugando Mwanza

baada ya hali zao kuwa mbaya.

Alisema madaktari wanaendelea kuwahudumia majeruhi hao

na hali zao zinaendelea vizuri baada ya wengine saba

kutibiwa na kuruhusiwa, huku akiwataka ndugu, jamaa na

marafiki kufika hospitalini hapo kwa ajili ya kutambua

miili ya marehemu ambao wamehifadhiwa chumba cha maiti

hospitalini hapo.

Kutokana na ajali hiyo mamia ya wananchi wamefulika

katika eneo la tukio wakisaidia kutoa miili ya marehemu

na majeruhi katika magari yaliyo gongana uso kwa uso

licha ya zoezi hilo kuwa gumu kutokana na ukosefu wa

vifaa vya kutoklea huduma ya kwanza .

Mkuu wa Wilaya ya Geita, Philemon shelutete na Mbunge wa

Jimbo la Busanda, Lolensia Bukwimba ambao wamefika eneo

la tukio na kueleza kusikitishwa na ajali hiyo na

kutamka ni janga la kitaifa, hivyo kuwataka Watanzania

kuomboleza juu ya vifo v ya wananchi hao.

Hata hivyo Shelutete amewataka wamiliki wa magari ya

abiria kuajiri madereva wenye ujuzi wa kutosha kwa lengo

la kupunguza ajali na kudai iwapo madereva hao

wangezingatia sheria za usalama ajali hiyo isinge tokea.