Wizara ya Fedha na Maonyesho ya Maadhimisho Miaka 50 ya Uhuru

*Katibu Mkuu Kiongozi atembelea Banda la Wizara ya Fedha leo

Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo akitoka kwenye banda la Wizara ya Fedha mara baada ya kutembelea Maonyesho ya Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere (Sabasaba) leo.

Katibu Mkuu Kiongozi, Philimon Luhanjo akitembelea banda la Wizara ya Fedha

Msemaeji Mkuu wa Wizara ya Fedha Bi. Ingiahedi Mduma akiwa tayari kuwakaribisha wageni mbalimbali wanaotembelea banda la Wizara ya Fedha katika Maonyesho ya Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere (Sabasaba).

Mchumi Mkuu Mwandamizi wa Wizara ya Fedha, ndugu Joseph Kiraia akifafanua jambo kwa wananchi waliotembelea banda la Wizara ya Fedha katika Maonyesho ya Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere (Sabasaba) leo.